Tuesday, September 27, 2016

Paka Mwindaji

Habari za siku tele wasomji wa makala zangu. Ni takribani mwezi sasa sijakutana na ninyi. Hili limetokana na changamoto za maisha.
Leo nataka kukuambia kuwa kama unataka kufanikiwa uwe kama Paka mwindaji. Paka mwindaji ukimkuta mahali anavizia kwenye shimo la panya utafurahi na pia utashangaa. Anaweza aka kaa hapo kwa zaidi ya saa moja. Ataziba pumzi ikiwezekana na mwisho atafanikiwa kwani panya atajitokeza akifikiri kuwa hakuna kitu kumbe! Paka namdaka na kumtafuna.
Mjasiriamali pia anatakiwa kuwa na uvumilivu mkubwa. Pamoja na mbinu/ ujuzi/ maarifa na kadhalika lakini UVUMILIVU ndicho kitu pekee kitakacho kuhakikishia mafanikio yako.
Usijali vikwazo utakavyo kutana navyo watu watakukatisha tamaa, watakubeza, watakuambia hauwezi au haiwezekani na wengine wataenda mbali zaidi na kutaka kukuondoa kwenye biashara. Lakini USIKATE Tamaa.
Kwa leo sina mengi.
Mika Hezekiele + Mwalimu