Sunday, August 28, 2016

NJIA Tano za Kutatua Matatizo

Habari za leo wapedwa wasomaji wa makalazangu.
Leo naomba tuzungumzie kwa ufupi juu yamatatizo na jinsi ya kuyakabili na kuyatatua.
Kwanza kabisa nataka ujuekuwa kama una tatizo basi usifikiri kuwa tatizo lako ni la kipekee sana na kuwa hakuna mtu mwingine aliye wahi kupitia hali ulio nayo! Ukweli ni kwamba watu kibao waliwahi kupitia hali kama ya kwako na jambo la kufurahisha walipapmbana na wakashinda.
Unaweza kusema kuwa hapa nilipofikia ni mwisho kabisa Ndiyo na mimi nakubali hapo ndo mwisho. Sasa geuka anza kurudi ulikotokea kwenye mafanikio.
Je, tunawezaje kutatua Tatizo?
1. Njia ya Kwanza
Unaweza kutumia mbinu yakulizunguka tatizo. Tatizo linaweza kuwa kama kikwazo cha njia a.k.a ROAD BLOCK sasa kama tatizo liko hivyo tafuta mbinu ya kulizunguka ili wewe uweze kupita na kuendelea na safari yko ya mafanikio.
2. Njia ya Pili ni kuchimba chini ya tatizo
Unaweza kuchimba chini ya tatizo lako kama lenyewe likombele yako kama mlima mrefu usioweza kuupanda. Chimba chini yake na utokee upande wa pili ili uweze kuendelea na safari yako ya mafanikio
3. Mbinu ya tatu ni kulipanda tatizo
Kama tatizo liko mbele yako kama mlima unaoweza kuupanda basi jikaze kiume uupande huo mlima wa tatizo ufike kileleni na mwisho unaelekea upande wa pili ukiwa mshindi.
4. Kabiliana na tatizo uso kwa uso
Matatizo mengine ni mabishi huwezi kufanikiwa kwa mbinu zote hizo hapo juu hivyo inabidi ukabiliane nalo uso kwa uso hadi umelishinda hilo tatizo.
Jambo la muhimu katika kukubaliana na tatizo usikabiliane na tatizo ukiwa mnyonge hakikisha unakua ngangari.
5. Uvumilivu
Uvumilivu unatakiwa pia na Imani inatakiwa ili uweze kuvuka vikwazo.
Asante sana.
Mika Ayo - Mwalimu

Monday, August 1, 2016

Leo Ni Muhimu Kwa Ajili Ya Kesho

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo napenda tuzungumzie juu ya mambo ambayo huwa tunafanya kila siku .
Ni muhimu kujua kuwa mambo ambayo tunayafanya kila siku yanaweza kukufanya ukafanikiwa au ukashindwa kusonga mbele maisha yako yote.
Mambo tunayofanya yanaweza kuonekana kama si mambo makubwa lakini yanaweza kuwa ya maana au yenye madhara kwetu.
Kwa mfano kutojisomea kunaweza kukufanya ukapitwa na wakati bila wewe kujua.Pia unajizuia kupata taarifa mpya ambazo zingeweza kubadilisha maisha yako na yakawa mazuri au yenye manufaa zaidi!
Suala la kutojisomea limekua tatizo kubwa kwenye jamii yetu hivi sasa.
Mfano mdogo tu ni kwa wanafunzi wetu wengi wa sekondari leo ukiwaambia wataje Mikoa ya Tanzania kwa kichwa hawawezi! Ukiwauliza sababu wanasema hawajafundishwa au wanakuambia hayo mambo yalikua muhimu zamani sio siku hizi. Hebu fikiria kijana wa karne ya 21 ambaye ana ndoto za kwenda Ulaya hajui hata kusoma ramani ya nchi yake achilia mbali ile ya Bara la Afrika.
Hii ndiyo sababu vijana wengi wamekua wakiiga mambo mabaya badala ya mambo mema. Kwanini. Vijana wanatumia leo yao kuzungumza, kuangalia kwenye intaneti na kusoma mambo ya udaku ambayo kwa kweli mara nyingi hubomoa badala ya kujenga.
Ndiyo maana vijana wengi wa kiume wamekuwa mashoga, wasichana wanafanya ngono bila kujua athari zake. Pia wanatumia madawa ya kulevya ulevi, kuvuta ugoro na kadhalika kwa sababu mambo hayo hayataki kuumiza akili.
Wanapenda walale masikini na kesho yake waamke wakiwa matajiri! Jambo hili haliwezekani. Najua kuna baadhi ya vijana wachache sana ambao wanajishughulisha kuboresha maisha yao kwa kufanya biashara halali, kazi halali na wengi wamefanikiwa na kwa kweli hawa nawapongeza sana.
Kwa wale ambao mnatumia leo yenu vibaya ninawaasa kubadilika. Hebu chukua hatua wewe mwenyewe anza kubadilika kidogo kidogo. Kwa mfano unaweza kuanza kujisomea vitabu vya ujasiriamali, uwekezaji, uchumi na vingine vingi.
Usitake kumaliza kitabu chenye kurasa mamia kwa mara moja "HAPANA" Soma kama nusu saa tu kwa siku moja halafu tafakari mambo au jambo ulilojifunza katika sura ya kitabu uliosoma. Fanya hivyo tena kesho yake. na kadhalika utashangaa utaanza kubadilika kimtazamo. Mazungumzo yako yatabadilika, tabia yako itabadilika. Hata aina ya marafiki zako watabadilika na mwisho watu wataanza kukuamini na hapo utakua tayari unaelekea kwenye mafanikio yako.
Kwa leo naomba niishie hapa niwatakia kila la heri katika kuiandaa kesho yenye mafanikio zaidi.

Mika Ayo:   Mwalimu 0673506836