Sunday, August 28, 2016

NJIA Tano za Kutatua Matatizo

Habari za leo wapedwa wasomaji wa makalazangu.
Leo naomba tuzungumzie kwa ufupi juu yamatatizo na jinsi ya kuyakabili na kuyatatua.
Kwanza kabisa nataka ujuekuwa kama una tatizo basi usifikiri kuwa tatizo lako ni la kipekee sana na kuwa hakuna mtu mwingine aliye wahi kupitia hali ulio nayo! Ukweli ni kwamba watu kibao waliwahi kupitia hali kama ya kwako na jambo la kufurahisha walipapmbana na wakashinda.
Unaweza kusema kuwa hapa nilipofikia ni mwisho kabisa Ndiyo na mimi nakubali hapo ndo mwisho. Sasa geuka anza kurudi ulikotokea kwenye mafanikio.
Je, tunawezaje kutatua Tatizo?
1. Njia ya Kwanza
Unaweza kutumia mbinu yakulizunguka tatizo. Tatizo linaweza kuwa kama kikwazo cha njia a.k.a ROAD BLOCK sasa kama tatizo liko hivyo tafuta mbinu ya kulizunguka ili wewe uweze kupita na kuendelea na safari yko ya mafanikio.
2. Njia ya Pili ni kuchimba chini ya tatizo
Unaweza kuchimba chini ya tatizo lako kama lenyewe likombele yako kama mlima mrefu usioweza kuupanda. Chimba chini yake na utokee upande wa pili ili uweze kuendelea na safari yako ya mafanikio
3. Mbinu ya tatu ni kulipanda tatizo
Kama tatizo liko mbele yako kama mlima unaoweza kuupanda basi jikaze kiume uupande huo mlima wa tatizo ufike kileleni na mwisho unaelekea upande wa pili ukiwa mshindi.
4. Kabiliana na tatizo uso kwa uso
Matatizo mengine ni mabishi huwezi kufanikiwa kwa mbinu zote hizo hapo juu hivyo inabidi ukabiliane nalo uso kwa uso hadi umelishinda hilo tatizo.
Jambo la muhimu katika kukubaliana na tatizo usikabiliane na tatizo ukiwa mnyonge hakikisha unakua ngangari.
5. Uvumilivu
Uvumilivu unatakiwa pia na Imani inatakiwa ili uweze kuvuka vikwazo.
Asante sana.
Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment