Wednesday, June 22, 2016

Kazi au Malipo?

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo naomba ujiulize je? Unacho kifanya ni kazi kwa ajili ya kutimiza hitaji fulani katika jamii au ni kazi kwa ajili ya kujipatia malipo au kipato?
Mimi sijuhi ila jibu unalo wewe lakini ngoja nikuambie faida na hasara za kufanya kazi kwa ajili ya malipo na kufanyakazi ili kujibu hitaji fulani ndani ya jamii.

Faida za kufanya kazi kwa ajili ya malipo

1. Utapata fedha kwa ajili ya mahitaji yako na watoto wako
2. Utalipwa unacho stahili
3. Utapata furaha ya muda mfupi sana
4. Utapata kazi

Hasara zake
1. Hutaridhika na kile unacholipwa kwani wewe unachotaka ni fedha na siyo kutoa huduma!
2. Utajenga maadui ndani na nje ya ofisi kwani wewe unachojali ni Pesa na siyo mahusiano na watu
3. Ukimaliza kazi utasahalika hutakumbukwa tena
4. Utakuwa mtu wa kujilaumu kila wakati

Faida ya Kufanya Kazi kama kazi
1. Utakuwa unajibu hitaji la jamii 
2. Utapata heshima kubwa na hutaweza kusahauliwa milele!
3. Utakuwa mwenye furaha maisha yako yote!
4. Utatimiza malengo yako siku zote
5. Utakuwa na marafiki ndani na nje ya ofisi yako.

Hasra za kufanya kazi kama kazi

1. Kutoa muda wako mwingi kwa ajili ya wengine
2.  Wale unaofanya kazi nao kukutegea kwani wanajua wewe hutakubali jahazi lizame
3. Unaweza kupoteza haki zako kutokana na kwamba wewe unachojali ni kutimiza wajibu wako na siyo malipo malipo kwako si kitu muhimu. La muhimu kwako ni kutimiza kazi yako.
Hivyo nakushauri uchukue hatua ufanye kazi kama kazi kwani hata kama watakudhulumu haki yako itapatikana au niseme utaipata tu!
Wewe wekeza kwenye jamii siku moja utalipwa hadi ushangae.
Mika Ayo - Mwalimu


Friday, June 17, 2016

Jinsi ya Kuepuka Mateso ya Baadaye

Habari za leo wasomaji wa makala zangu
Kwanza nawashukuru sana kwa kusoma kile ambacho nakiandika humu. Leo naomba niwape siri kwa nini nimeamua kumiliki blogu yangu mwenyewe!
NI ILI NIPATE UHURU WA KIFEDHA 
Mimi niko tayari kuteseka kwa ajili ya kupata UHURU kamili. Robert Kyosaki mwandishi mashuhuri sana na tajiri na rafiki mkubwa wa Mgombea urais wa Marekani Donald Trump aliwahi kusema. Freedom is not real freedom without financial freedom! Rich Dad Poor Dad by Robert Kyosaki
Mimi nimeianza safari hii nikiwa na Miaka zaidi ya 50!
Hii ni kutokana na kuchelewa kupata taarifa sahihi mapema au basi kwa kuwa mimi ni muumini mzuri wa dini yangu ya Kikristo nisema huu ndiyo mpango wa Mungu kwangu.
Ni meamua kuteseka kwa kuacha kazi serikalini hivyo sina kiinua mgongo (tangu mwanzo nilichukia na hata sasa nachukia dhana ya kiinua mgongo na pensheni! Kimsingi sikubaliani na kulipwa mamilioni baada ya mateso ya maisha yote, umenyanyaswa na bosi mchana kutwa jioni mwenyenyumba unaye, watoto wamefukuzwa shule ada hujalipa n.k eti baada ya mateso yote hayo unapewa shilingi milioni 60 ukiwa na miaka 60! Ili uifanyie nini? ujenge nyumba au ununue matatizo? Maana hukuwahi kushika kiasi kikubwa cha hela maisha yako yote. Ninaamini hutaweza kuimiliki na ndiyo maana wastaafu wengi wanafilisika chini ya miaka miwili hawana kitu!)
Najua stori za akina Colonel Harland David Sanders Wa Kentucky Fried chicken alianza safari hii akiwa na zaidi ya miaka 60 na alifika.
Wako walioanza na miaka zaidi ya 70 wakafika hivyo sina shaka mimi pia nitafika.
Najua kwa msaada wa watu waliofanikiwa  sina shaka nitafika cha msingi ni mimi kutokata tamaa.
Pia hata wewe nakushauri usikate tamaa. Njoo tushauriane nini cha kufanya. Usiache kazi kama umeahiriwa wewe fanya lakini uwe na malengo ya maisha hakikisha fedha yako inakufanyia kazi kwa bidii. Kama hujui jinsi ya kuifanya fedha ikufanyie kazi ili ikuzalishie fedha nyingi zaidi uliza kwa watu utapata ushauri wa nini cha kufanya.
Nashukuru sana kocha. Ubarikiwe
Mika Ayo

Saturday, June 11, 2016

UMUHIMU WA KUFANYA UTAFITI

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo nataka nizungumze kwa kifupi juu ya utafiti na umuhimu wake kabla hujawekeza.
Utafiti utakusaidia kujua mambo kadhaa katika biashara au shughuli unayo taka kuwekeza.
Watu wengi huanzisha biashara kabla ya kujua ugumu na changamoto zilizoko kwenye biashara husika!
Watu hujiiingiza kwenye biashara eti kwa kuwa tu ndugu au rafiki yao fulani amefanikiwa kwenye biashara hiyo.
Ngoja nikupe siri moja. HAKUNA MTU ATAKAYE KUONA UKIWA CHINI NAMAANISHA KABLA YA KUFANIKIWA. Mara zote watu watakuona pale unapofanikiwa na huwa hawakumbuki umeteseka miaka mingapi au ni magumu mangapi umepitia kabla ya kufikia hapo ulipo. Wao hufikiri ni rahis kufanikiwa hivyo hukurupuka na baadaye wanapata hasara.
Ili usipate hasara ya muda na fedha na mwisho kukata tamaa na maisha ni vizuri ukafanya utafiti wa kutosha juu ya biashara yako mpya unayotaka kuanzisha.
Utafiti utakusaidia mambo yafuatayo ( haya ni machache kati ya mengi)
i) Kujua ukubwa au udogo wa soko la bidhaa zako
ii) Kujua washindani wako katika biashara na nguvu walionayo kwenye biashara husika
iii) Kujua watu wa kukusaidia ili uweze kuanza biashara husika
iv) Kuamua mchepuo (niche) wa biashara yako kwa mfano kama unataka kuanzisha biashara ya huduma ya kuhudumia watalii basi unaweza kuangalie wewe ujikite kwenye mchepuo gani kutokana na vigezo ulivyo navyo wewe
v) Kujua masuala ya kisheria yahusuyo biashara husika
vii) Kujua hitaji ambalo bado halijatoshelezwa kwenye biashara husika (hii inaweza kuwa ndiyo nguvu na nguzo muhimu sana kwako ambayo itakupa mafanikio kwani utakuwa unawasaidia watu kutatua matatizo au tatizo ambalo bado halijatatuliwa na ukiweza kutoa ufumbuzi basi umepiga BINGO)
viii) Kujua pa kuanzia na mengine mengi
Hivyo nakushauri ndugu yangu usikurupuke kuanza biashara wewe fanya utafiti kwanza ndipo uchukue maamuzi kutokana na taarifa ulizo kusanya kwenye utafiti wako.
Asanteni
Mika Ayo - Mwalimu

Wednesday, June 8, 2016

SIKU ZAENDA MBIO

Japo mwaka wa kesha lakini siku zaenda,
Utadhani bado tupo na muda kumbe siku zaenda,
Huwezi kujua wewe ila siku zaenda
Utakapo lipwa mshahara au siku ya jambo hufika!
Hapo ndipo utatambua kumbe siku zaenda!
Juzi ilikuwa ndo jana na kesho ndo leo!
Kwanini kupoteza wakati na kumbe siku zaenda.
Jitume wa kwetu jitume kwani siku zaenda.
Juzi nilikuwa mtoto na jana nilikuwa baba eti leo mimi BABU!
Ni kwambiayo ni kweli kwani siku zaenda mbio sana!
Jitahidi kutimiza malengo kwani siku zaenda.
Huwezi kuja fidia siku ikishaenda imeenda!

Mika Ayo - Mwalimu ( 0763506835)