Friday, June 17, 2016

Jinsi ya Kuepuka Mateso ya Baadaye

Habari za leo wasomaji wa makala zangu
Kwanza nawashukuru sana kwa kusoma kile ambacho nakiandika humu. Leo naomba niwape siri kwa nini nimeamua kumiliki blogu yangu mwenyewe!
NI ILI NIPATE UHURU WA KIFEDHA 
Mimi niko tayari kuteseka kwa ajili ya kupata UHURU kamili. Robert Kyosaki mwandishi mashuhuri sana na tajiri na rafiki mkubwa wa Mgombea urais wa Marekani Donald Trump aliwahi kusema. Freedom is not real freedom without financial freedom! Rich Dad Poor Dad by Robert Kyosaki
Mimi nimeianza safari hii nikiwa na Miaka zaidi ya 50!
Hii ni kutokana na kuchelewa kupata taarifa sahihi mapema au basi kwa kuwa mimi ni muumini mzuri wa dini yangu ya Kikristo nisema huu ndiyo mpango wa Mungu kwangu.
Ni meamua kuteseka kwa kuacha kazi serikalini hivyo sina kiinua mgongo (tangu mwanzo nilichukia na hata sasa nachukia dhana ya kiinua mgongo na pensheni! Kimsingi sikubaliani na kulipwa mamilioni baada ya mateso ya maisha yote, umenyanyaswa na bosi mchana kutwa jioni mwenyenyumba unaye, watoto wamefukuzwa shule ada hujalipa n.k eti baada ya mateso yote hayo unapewa shilingi milioni 60 ukiwa na miaka 60! Ili uifanyie nini? ujenge nyumba au ununue matatizo? Maana hukuwahi kushika kiasi kikubwa cha hela maisha yako yote. Ninaamini hutaweza kuimiliki na ndiyo maana wastaafu wengi wanafilisika chini ya miaka miwili hawana kitu!)
Najua stori za akina Colonel Harland David Sanders Wa Kentucky Fried chicken alianza safari hii akiwa na zaidi ya miaka 60 na alifika.
Wako walioanza na miaka zaidi ya 70 wakafika hivyo sina shaka mimi pia nitafika.
Najua kwa msaada wa watu waliofanikiwa  sina shaka nitafika cha msingi ni mimi kutokata tamaa.
Pia hata wewe nakushauri usikate tamaa. Njoo tushauriane nini cha kufanya. Usiache kazi kama umeahiriwa wewe fanya lakini uwe na malengo ya maisha hakikisha fedha yako inakufanyia kazi kwa bidii. Kama hujui jinsi ya kuifanya fedha ikufanyie kazi ili ikuzalishie fedha nyingi zaidi uliza kwa watu utapata ushauri wa nini cha kufanya.
Nashukuru sana kocha. Ubarikiwe
Mika Ayo

No comments:

Post a Comment