Thursday, October 20, 2016

Mbingu Na Ardhi

Wapendwa wasomaji wa makala zangu. Habari za leo.
Leo napenda tutafakari juu ya Mbingu na Ardhi. Mbingu ziko juu sana  naweza kusema kuwa hazishikiki ama hazifikiki! Kwa wale waliowahi kupanda Ndege ama kukwea Pipa kama wengine wapendavyo kuita   ni mashahidi kuwa kwa kadri unavyoenda juu unaona ni kama mbingu zinasogea kwenda juu zaidi. Ila cha kufurahisha ni kwamba kuna wakati ukipanda juu usawa wa mawingu basi utayafikia mawingu, ungeweza kupaa kiwango cha kufikia nyota ungezifikia nyota kama vile mwezi, Mars na kadhalika.

Ardhi ni mahali ambapo tuna cheza karibu kila siku saa 24 siku saba za wiki. Tunapanda mazao juu ya ardhi tunajenga juu ya ardhi, tunasafiri juu ya ardhi na kadhalika.

Sasa leo naona tutafakari kuwa Mbingu ni yale mategemeo au ndoto zetu za Juu sana tutakazo kuzifikia. Ardhi ni mambo ambayo ni kawaida kuyafanya na hakuna mtu anayeshindwa kuyafanya. Kwa kweli hata nyani wanaweza kuyafanya ila SHUGHULI IKO KUZIFIKIA MBINGU. YAANI MALENGO MAKUBWA.
Yafaa kujua kuwa tunahitaji nguvu na akili ya ziada ili kuyafikia mawingu au nyota.
Tunatakiwa kujitahidi maana kukutembea juu ya ardhi inahitaji juhudi.
Lakini kupaa kwenda mbinguni kunahitaji jitihada za hali ya juu sana.
Usikubali kulingana na nyani pambana uwe kama ndege Tai yeye hupaa juu kuliko ndege wote ingawa baadaye hurejea katika ardhi.
Kazi ni Kwakwo
Mwalimu Mika Ayo 

Sunday, October 2, 2016

Moyo wa shukrani

Kushukuru ni vema sana, tena yafurahisha moyo
Uso wako utakunjuka mara unapo shukuru
Tena utachangamka pindi unaposhukuru
Unapata na nyongeza pale unapo shukuru
Wala hakutoi moyoni yeye uliye mshukuru
Wala hapana kufuru pale unapo shukuru
Tena kuna uhuru wa kweli pale unapo shukuru
Hubaki hata na deni iwapo umeshukuru
Shukuru kila wakati Mola kaagiza tushukuru
Tena kwa kila tendo kiduchu pia shukuru
Lau kana maudhi hebu wewe shukuru
Kwani kulipa ubaya ? wewe nenda shukuru
Wala usione haya kusema asante tena nashukuru
Usiache kushukuru japo mara moja kwa siku shukuru

Wasalaam
Mwl. Mika Ayo