Tuesday, November 15, 2016

Saa 12 za Usiku ( Wimbo wa Mlinzi)

Sikieni ndugu zangu saa ya kwanza imefika " Mmoja ndiye Mwenyenzi na Mwokozi shidani"
Kibwagizo:
Watu hukaa macho bure, Mungu ndiye mwenye kukesha Bwana twakuomba we, utulinde usiku huu.
 
Sikieni ndugu zangu saa ya pili imefika " Njia ziko mbili tu, Uchague Nyembamba"

Sikieni ndugu zangu saa ya tatu imefika " Tukumbuke utatu; Baba, Mwana na Roho"

Sikieni nduku zangu saa ya nne imefika "Namna nne udongo zingatieni ndugu"

Sikieni Ndugu zangu saa ya tano imefika " Wanawali watano ndiyo wenye busara"

Sikieni ndugu zangu saa ya sita imefika " Ulimwengu wa Umbwa siku sita na Bwana"

Sikieni ndugu zangu saa ya saba imefika "tukumbuke maneno yale ya msalabani"

Sikieni ndugu zangu saa ya nane imefika " Waliwekwa dhamana gharikani mwa maji"

Sikieni ndugu zangu saa ya tisa imefika " Walirudi nyumbani tisa bila shukrani"

Sikieni ndugu zangu saa ya kumi imefika " Amri kumi za Mungu zishikeni ee Ndugu"

Sikieni ndugu zangu Edashara imefika " edashara walibaki waminifu kwa Bwana"

Sikieni ndugu zangu " Thenashara imefika, Thenashara ni mwisho nyota zote zatoweka giza litarudi tena tumshukuruni Mungu amekesha usiku huu.

Mika Ayo 

Sikieni

Wednesday, November 2, 2016

KWA NINI HUNA SHUKURANI?

Wapenzi wasomaji wa makala zangu, karibuni sana kwenye jamvi!
Leo nataka kuuliza swali moja tu, nalo ni hili hapa
"KWA NINI HUNA SHUKURUANI"? 
Msingi wa swali langu ni kutokana na wewe au wenzio kuzisoma makala zangu na kunyamaza kimya kama hakuna kilichotokea!
Ukweli ni kwamba watu huwa wanasoma au kutembelea Blogu yangu tangu nilipoifungua mwezi wa Tatu mwaka huu wa 2016. 
Hadi sasa ikiwa imefika mwezi wa Kumina moja ni takribani wa tu zaidi ya 1000 wamesha itembelea. Cha kushangaza ni kwamba hakuna hata mmoja aliwahi hata kunikosoa kama naandika vitu havifai au pengine vyenye kuleta tija kwa Jamii.
Leo naamua kusema ili watu wajirekebishe. Yamkini wengi hufika hapa kwa bahati mbaya wanapo pekua mtandao kupitia gwiji letu la Google.com ama vinginevyo. Lakini nikiangalia idadi ya watu walio wahi kutembelea Blogu yangu ni wastani wa watu mia moja kwa mwezi. Hata kama baadhi yao wakifika hawasomi lakini ninaamini kuwa kunao wanao soma makala zangu. Haiwezekani watu mia kwa mwezi wakafika hapa na wote wakapiga teke wasisome hilo haliniingii akilini kabisa!
Ninacho kuomba wewe utakayesoma makala hii hebu sema kitu chochote. Niko tayari kukusikiliza hata kama siyo kitu cha kunifurahisha alimradi ni jambo la kunijenga ili niweze kuandika makala nzuri na zenye nguvu zaidi basi mimi nitakushukuru sana.
Ukifanya hivyo utakuwa UMENIPA SHUKURANI AMBAYO SIJAWAHI KUIPATA.
Karibu sana nakusubiri.
Mika Ayo Mwalimu (0763506835 au 0673506836)