Wednesday, November 2, 2016

KWA NINI HUNA SHUKURANI?

Wapenzi wasomaji wa makala zangu, karibuni sana kwenye jamvi!
Leo nataka kuuliza swali moja tu, nalo ni hili hapa
"KWA NINI HUNA SHUKURUANI"? 
Msingi wa swali langu ni kutokana na wewe au wenzio kuzisoma makala zangu na kunyamaza kimya kama hakuna kilichotokea!
Ukweli ni kwamba watu huwa wanasoma au kutembelea Blogu yangu tangu nilipoifungua mwezi wa Tatu mwaka huu wa 2016. 
Hadi sasa ikiwa imefika mwezi wa Kumina moja ni takribani wa tu zaidi ya 1000 wamesha itembelea. Cha kushangaza ni kwamba hakuna hata mmoja aliwahi hata kunikosoa kama naandika vitu havifai au pengine vyenye kuleta tija kwa Jamii.
Leo naamua kusema ili watu wajirekebishe. Yamkini wengi hufika hapa kwa bahati mbaya wanapo pekua mtandao kupitia gwiji letu la Google.com ama vinginevyo. Lakini nikiangalia idadi ya watu walio wahi kutembelea Blogu yangu ni wastani wa watu mia moja kwa mwezi. Hata kama baadhi yao wakifika hawasomi lakini ninaamini kuwa kunao wanao soma makala zangu. Haiwezekani watu mia kwa mwezi wakafika hapa na wote wakapiga teke wasisome hilo haliniingii akilini kabisa!
Ninacho kuomba wewe utakayesoma makala hii hebu sema kitu chochote. Niko tayari kukusikiliza hata kama siyo kitu cha kunifurahisha alimradi ni jambo la kunijenga ili niweze kuandika makala nzuri na zenye nguvu zaidi basi mimi nitakushukuru sana.
Ukifanya hivyo utakuwa UMENIPA SHUKURANI AMBAYO SIJAWAHI KUIPATA.
Karibu sana nakusubiri.
Mika Ayo Mwalimu (0763506835 au 0673506836)

No comments:

Post a Comment