Sikieni ndugu zangu saa ya kwanza imefika " Mmoja ndiye Mwenyenzi na Mwokozi shidani"
Kibwagizo:
Watu hukaa macho bure, Mungu ndiye mwenye kukesha Bwana twakuomba we, utulinde usiku huu.
Sikieni ndugu zangu saa ya pili imefika " Njia ziko mbili tu, Uchague Nyembamba"
Sikieni ndugu zangu saa ya tatu imefika " Tukumbuke utatu; Baba, Mwana na Roho"
Sikieni nduku zangu saa ya nne imefika "Namna nne udongo zingatieni ndugu"
Sikieni Ndugu zangu saa ya tano imefika " Wanawali watano ndiyo wenye busara"
Sikieni ndugu zangu saa ya sita imefika " Ulimwengu wa Umbwa siku sita na Bwana"
Sikieni ndugu zangu saa ya saba imefika "tukumbuke maneno yale ya msalabani"
Sikieni ndugu zangu saa ya nane imefika " Waliwekwa dhamana gharikani mwa maji"
Sikieni ndugu zangu saa ya tisa imefika " Walirudi nyumbani tisa bila shukrani"
Sikieni ndugu zangu saa ya kumi imefika " Amri kumi za Mungu zishikeni ee Ndugu"
Sikieni ndugu zangu Edashara imefika " edashara walibaki waminifu kwa Bwana"
Sikieni ndugu zangu " Thenashara imefika, Thenashara ni mwisho nyota zote zatoweka giza litarudi tena tumshukuruni Mungu amekesha usiku huu.
Mika Ayo
Sikieni
No comments:
Post a Comment