Tuesday, November 15, 2016

Saa 12 za Usiku ( Wimbo wa Mlinzi)

Sikieni ndugu zangu saa ya kwanza imefika " Mmoja ndiye Mwenyenzi na Mwokozi shidani"
Kibwagizo:
Watu hukaa macho bure, Mungu ndiye mwenye kukesha Bwana twakuomba we, utulinde usiku huu.
 
Sikieni ndugu zangu saa ya pili imefika " Njia ziko mbili tu, Uchague Nyembamba"

Sikieni ndugu zangu saa ya tatu imefika " Tukumbuke utatu; Baba, Mwana na Roho"

Sikieni nduku zangu saa ya nne imefika "Namna nne udongo zingatieni ndugu"

Sikieni Ndugu zangu saa ya tano imefika " Wanawali watano ndiyo wenye busara"

Sikieni ndugu zangu saa ya sita imefika " Ulimwengu wa Umbwa siku sita na Bwana"

Sikieni ndugu zangu saa ya saba imefika "tukumbuke maneno yale ya msalabani"

Sikieni ndugu zangu saa ya nane imefika " Waliwekwa dhamana gharikani mwa maji"

Sikieni ndugu zangu saa ya tisa imefika " Walirudi nyumbani tisa bila shukrani"

Sikieni ndugu zangu saa ya kumi imefika " Amri kumi za Mungu zishikeni ee Ndugu"

Sikieni ndugu zangu Edashara imefika " edashara walibaki waminifu kwa Bwana"

Sikieni ndugu zangu " Thenashara imefika, Thenashara ni mwisho nyota zote zatoweka giza litarudi tena tumshukuruni Mungu amekesha usiku huu.

Mika Ayo 

Sikieni

No comments:

Post a Comment