Thursday, May 18, 2017

JINSI YA KUFANYA BIASHARA YA MTANDAO

Habari za leo ndugu zangu.
Leo nataka tuzungumze kwa kifupi juu ya biashara ya MTANDAO. Baadhi ya watu wakisikia biashara ya "mtandao" hufikiri kuwa kinacho zungumzwa ni biashara ya mtandao wa kompyuta! Kumbe! Sio kabisa. Ingawa komputa kupitia intaneti, pia simu kupitia kile kinachoitwa mitandao ya kijamii huweza kuwaunganisha watu na wakafanya mtandao wa namna moja ama nyingine lakini Biashara ya Mtandao ni kitu tofauti kabisa.

Biashara ya Mtandao ni Nini?
Biashara ya mtandao ni mtindo wa kuuza bidhaa au huduma kwa njia ya mtu mmoja kumshirikisha mtu mwingine kwa njia ya mdomo au email au njia yoyote nyingine bila kuwepo kwa mtu wa kati yaani middle man na kama aliye shirikishwa akikubali hujiunga kwenye biashara chini ya ulezi wa yule aliye mwalika. Mara nyingi mwanachama ambaye hujulikana kama msambazaji wa kampuni fulani huwa ndiye: Mteja namba moja wa bidhaa au huduma anazo uza au kusambaza. Pia yeye huwa ndiye Bango la matangazo la kampuni anayoiwakilisha. Hivyo basi huu ni mtandao (muunganiko wa watu) unaofanyakazi pamoja ili kutimiza malengo yao tofauti ingawa wote wako kwenye biashara moja. Kwa kifupi Biashara ya Mtandao ni muunganiko wa watu wanaotumia, kuingiza wanachama wapya na kusambaza bidhaa za kampuni husika.

Ni Nini Watu Wengi Wasichoelewa kwenye Biashara ya Mtandao?
Jambo moja linalo watesa wasambazaji wengi kwenye biashara ya mtandao ni kutumia mtindo wa kibiashara walio uzoea kwenye biashara za kawaida na kuuleta kwenye biashara ya mtandao. Hapa ninamaana kuwa watu wengi huwekeza nguvu kubwa kwenye kuuza zaidi kuliko kusajili.
Tatizo hili linatokana na watu wengi kutokujua hasa ni nini madhumuni ya msingi ya biashara ya mtandao.

Dhumuni kubwa la biashara ya Mtandao ni kuhakikisha kuwa una watu wengi wanokufanyia kazi yaani ningeweza kuwaita wafuasi wako au huitwa down liners kwa kingereza. Kwa kuwa moja ya lengo kubwa la biashara ya mtandao ni kuhakikisha kuwa kila mtu aliyejiunga anatumia kwanza bidhaa/ huduma za kampuni basi kadri unapokuwa na wafuasi wengi basi hata bila kuuza utajikuta kuwa umepata fedha ya kutosha kwenye biashara yako kutokana na manunuzi ya kawaida ya timu yako au wafuasi wako.
NB: Usije ukaichukia biashara hii kwa kuona kama utakuwa unamfanyia mtu kazi la! kazi yoyote unayoifanya ni kwa manufaa yako 100% kwani ukiuza bidhaa unalipwa, ukiingiza mwanacha mpya kwenye biashara unalipwa na baadaye mwisho wa siku kampuni inakupa gawio la faida waliopata. Ni tofauti kabisa na biashara za kawaida ambapo pia hawa watu wenye makampuni ya bidhaa tunazo uza kama vile sukari, soda, nguo nk huwa tunawafanyia kazi na tunachokipata ni lile punguzo la bei ambalo tutalipata kupitia kwa wateja wetu. Basi hakuna kingine!
 
Mfano kama timu yako ina watu 10,000 na watu hawa wakanunua bidhaa za wastani wa shilingi 20,000 kwa mwezi kwa kila mmoja na tuseme kampuni ina sera ya kulipa fidia ya asilimia 5% kwa mauzo ya timu yako hapa utapata TZS 10,000,000 kwa mwezi na pengine wewe umenunua bidhaa za TZS 200,000 kwa mwezi husika!

Hivyo kazi kubwa ni kuandikisha/ kusajili wanachama wapya kuliko kuuza. Kwa nini kuuza kwanza usingeweza kuuza peke yako kiasi hicho kikubwa cha bidhaa kwa mwezi. Pili hata kama unaweza kuuza bidhaa ambazo zinakuwezesha kujikimu kimaisha kwa kipindi fulani, bado una kuwa umekiuka malengo ya biashara ya mtandao. Kwa nini hii inakuweka uwe sawa na mtu mwenye maduka au biashara za kawaida au waajiriwa! Hili siyo lengo, lengo la biashara ya mtandao ina lenga kukuwezesha kuingiza fedha kama unafanya kazi au unaumwa bado fedha zinaingia alimradi tu uwe umesha pata wafuasi au timu kubwa ya kutosha yaani kipato kikubwa kwa kazi kidogo!.

Mbinu zifuatazo zinaweza kukusaidia

a) Onyesha Fursa
Watu wengi hawawezi kunyesha fursa ilioko kwenye biashara ya mtandao. Mtu akigundua kuwa kama akiweka muda wake hapo mwisho wa siku atajikwamua kimaisha basi wangeipokea biashara hiyo na kunufaika na fursa zilizopo

b) Ongea na watu wengi iwezekanavyo
Haitoshi tu kuongea na watu wachache ongea na watu wengi iwezekanavyo.
Jifunze kukataliwa bila kukata tamaa. Watu wengi huchukia au kuogopa kuendelea kuonyesha fursa pale wanapo kataliwa. Siri hapa ni kuendelea ujue kuwa kati ya watu 100 utakaowaambia fursa yako 10 watasikiliza, 5 watataka kujua zaidi na pengine 2 tu ndiyo watakaojiunga! Hivyo jipange na usikate tamaa.

c) Usiache kujifunza.
Kitu kingine watu wengi hufikiri kuwa wanajua kila kitu na hawana haja ya kujifunza. Kumbe wanapotea. Kila siku kunamabadiliko na ili uweze kuendana na mabadiliko unatakiwa kujifunza kila mara.
Nikutakie mafanikio mema kwenye BIASHARA YAKO YA MTANDAO.
Jaribu hii hapa
http://bitcoinslip.com/?hash=36546

Asanteni sana ni mimi
Mwalimu
Mika Ayo

Wednesday, May 17, 2017

JINSI YA KUITAMBUA 'FURSA'

Habari za leo ndugu zangu. Ni siku nyingi hatujaongea kwenye huu ukurasa. Nimekuwa na mambo mengi kiasi kwamba wasomaji wangu mnakosa uhondo wa mazungumzo haya.

'FURSA' NI NINI?
 
Leo nataka kuzungumzia maana ya 'FURSA'
Nadhani kila mtu ukimuuliza maana ya hili neno 'FURSA' atakupa tafsiri yake. Na kwangu mimi kila tafsiri inaweza kuwa sahihi kutokana na kila mtu anavyolielewa neno 'FURSA'

Kwangu mimi fursa ni JINSI MTU ANAVYOWEZA kutazama jambo au kitu na kubuni manufaa yake au ya jamii kubwa kutokana na Jambo au Kitu anachokitazama , alichokiona au alichofikiri.
Ni rahisi sana kusikia watu wakisema katika mji fulani au kijiji fulani hakuna 'FURSA'  ya hili au lile. Hii ni kwa sababu tayari wao wanamtazamo au wanacho walicho tarajia kukiona ambao kwao wao ndio 'FURSA' lakini kwangu mimi hakuna mahali kokote duniani hapa ambapo hapana 'FURSA' Tatizo ni kwamba tu, bado hatujafikiri na kutafuta kwa kina juu ya eneo au hali husika ndiyo maana bado hatujaona 'FURSA' iliyopo mahali au katika hali husika.
Ngoja nikupe mifano hai mitatatu (hii ni mifano ya wazi kabisa)

1.  Uwepo wa Bahari
Hapa Tanzania tunayo bahari ya Hindi. Sasa hebu nikupe jinsi watu tofauti wanavyo itazama Bahari hii kama 'FURSA':

a) Wavuvi

 Kwao ni fursa ya kupata samaki kwa ajili ya kitoweo chao na familia na pia watawauzia watu na kupata fedha kwa ajili ya matumizi mengine.

b) Mabaharia 
Wataiona Bahari kama fursa ya kusafirisha abiria na mizigo kwenda nchi nyingine na wao kujipatia kipato kwa ajili ya kazi hiyo.

c) Wafanya biashara ya utalii
Wataona fukwe za Bahari kama mahali pazuri pa kujenga hoteli na pia kuwapeleka watalii na kujipatia fedha. Orodha inaweza kuwa ndefu lakini naomba niishie hapa kwanza.

2. Uwepo wa miji
Hapa kwetu Tanzania pia kuna miji mingi tu ingawa inatofautiana kwa ukubwa lakini watu mbalimbali wanaweza kuona 'FURSA' mbalimbali kama ifuatavyo:

a) Wasafirishaji wa Abiria na mizigo
Kutokana na kuwepo kwa mkusanyiko mkubwa wa watu wasafirishaji wataona kuna fursa ya kusafirisha ABIRIA na mizigo.

b) Watu wa Elimu
Hawa wataona 'FURSA' ya kufungua shule, vyuo na taasisi mbalimbali za kutoa elimu

c) Watu wa Afya
Hawa wataona 'FURSA' ya kufungua hospitali na maduka ya dawa nakadhalika.

Hivyo kabla ya kulalamika hebu bunga bongo kidogo inawezekana hapo ulipo iko 'FURSA' inayokusubiri uitambue ili uweze kubadilisha maisha yako na ya jamii nzima.

tembelea hapa kwenye mtandao huu na ujiandikishe inaweza kukusaidia.

http://bitcoinslip.com/?hash=36546


KARIBU SANA
Mika Ayo
Mwalimu

Wednesday, May 3, 2017

Jinsi ya Kupambana na Woga

1. Toka Nje ya Chumba/ Nyumba

Haiwezekani kuwaza vizuri wakati umejawa na hofu na wasiwasi. Jambo la kwanza la kufanya ni kutoka nje na kukaa kwa muda nje ya mazingira yako ya kawaida hadi utakapo tulia kabisa.
Jipe mapumziko ya dakika 15 mbali na jambo linalokupa hofu au woga kwa kutembea kuzunguka jengo la ofisi/nyumba unaweza pia kunywa chai au unaweza hata kwenda kuoga.

2. Vuta Hewa Nyingi

Kama moyo unakuenda mbio au jasho linaanza kutoka kwenye viganja usijaribu kuzuia.
Baki palepale na endelea kujisikilizia bila kushughulikia hali hiyo.
Baada kama dakika moja ama mbili weka kiganja cha mkono wako tumboni na anza kuvuta hewa taratibu, kwa kuvuta hewa ndani kwa wengi kuliko kawaida na kuiachia itoke nje taratibu.
Lengo ni kujaribu kuzisaidia akili zako kuzoea hali ya mashaka iliyojitokeza na kuweza kuchukuliana na hali halisi na baadaye kuondoa hofu.
Kama unaweza tembelea breathing technique for stress.

3. Kabili Unachokiogopa

Kujidai kutojali huweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi. Lolote linalo kutatiza na kukuogopesha kama utaamua kulikabili huanza kuonekana jambo la kawaida. Kama kuna siku ulipata woga kutumia lifti au kuvuka daraja refu jaribu kurudia tena na tena hadi utazoea. Fanya hivi kila siku na utaona limekuwa ni jambo lakawaida.

4. Fikiria Jambo Gumu na Baya kukupata

Unaweza kufikiri kuwa unakaribia kupata ugonjwa wa moyo – labda ni kutojiamini tu kuwa utapata ugonjwa wa moyo. Halafu anza kuwaza kuwa wewe huwezi kabisa kwa njia yoyote kupata ugonjwa kama huo. Jitahidi kukabiliana na woga utashangaa woga na hofu vitaondoka.

5. Ikabili Hali Halisi

Huwa wakati mwingine ni vizuri kukabilianan na mawazo ya woga, Kwa mfano unaweza kufikiri kuwa unaweza kukwama kwenye ngazi ya umeme (lift) ya kupanda ghorofani na ukakosa hewa na kufa! Lakini jaribu kujihoji je, uliwahi kusikia mtu aliye pata na mkasa kama huo? Na je kama unaye rafiki mwenye hofu kama hiyo ungemsaidiaje? Jitahidi kuondoa Uoga wa namna yoyote na utashangaa hofu itaondoka na utakuwa huru.

6. Usijaribu Kujifanya Sahihi wakati wote

Maisha yamejaa changamo, ingawa wengi wetu hujihisi kuwa kuwa maisha yao yangekuwa sahihi. Ujue tu kuwa siku mbaya na vikwazo viko siku zote hivyo ni vizuri kujua kuwa maisha ni mchakamchaka.

7. Waza Kama Uko Mahali Pazuri


Hebu kwa dakika moja fumba macho na fikiria kwamba huko mahali pazuri na salama na palipo tulia. Inaweza kuwa unawaza kwamba unatambea ufukweni au uko kitandani na paka (kama wewe ni mpenzi wa wanyama hao) au unaweza kujikumbusha jambo ambalo lilikufurahisha sana wakati wa utoto acha hisia hizo nzuri zikufunike hadi ujisikie mwepesi.

8. Ongea

Ukimwambia mtu wako wa karibu kuhusu hofu yako husaidia sdana kupunguza hofu na woga. Kama huna wa kuongea naye nenda kwa mnasihi hawa wanapatikana hasa kwenye ngazi ya Hospitali za Wilaya au kwenye baadhi ya Mashirika yasiyo ya serikali NGO. Au unaweza kutembelea Idara za Usatawi wa Jamii Ngazi ya Wilaya watakusaidia.

9. Fanya Mambo ya Kawaida

Watu wengi hurudia ulevi au hata madawa ya kulevya kama njia ya kuondoa hofu, lakini jambo hili laweza likakufanya ukachanganyikiwa zaidi. Jaribu kufanya mambo ya kawaida kila siku kama vile kujitahidi kulala vizuri kupata mlo kamili, kufanya mazoezi angalao dakika 30 kwa siku na kupumzika hili linaweza kuondoa msongo wa mawazo.

10. Jipongeze

La mwisho hebu jipongeze. Unapofanikisha jambo lolote katika maisha yako hebu jipongeze kwa kujipa zawadi. Nenda kwenye hoteli nzuri jinunulie chakula unachopenda au fanya jambo lolote linalokupa furaha hii husaidia sana kuondoa kutojiamini na Hofu.