Wednesday, June 22, 2016

Kazi au Malipo?

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo naomba ujiulize je? Unacho kifanya ni kazi kwa ajili ya kutimiza hitaji fulani katika jamii au ni kazi kwa ajili ya kujipatia malipo au kipato?
Mimi sijuhi ila jibu unalo wewe lakini ngoja nikuambie faida na hasara za kufanya kazi kwa ajili ya malipo na kufanyakazi ili kujibu hitaji fulani ndani ya jamii.

Faida za kufanya kazi kwa ajili ya malipo

1. Utapata fedha kwa ajili ya mahitaji yako na watoto wako
2. Utalipwa unacho stahili
3. Utapata furaha ya muda mfupi sana
4. Utapata kazi

Hasara zake
1. Hutaridhika na kile unacholipwa kwani wewe unachotaka ni fedha na siyo kutoa huduma!
2. Utajenga maadui ndani na nje ya ofisi kwani wewe unachojali ni Pesa na siyo mahusiano na watu
3. Ukimaliza kazi utasahalika hutakumbukwa tena
4. Utakuwa mtu wa kujilaumu kila wakati

Faida ya Kufanya Kazi kama kazi
1. Utakuwa unajibu hitaji la jamii 
2. Utapata heshima kubwa na hutaweza kusahauliwa milele!
3. Utakuwa mwenye furaha maisha yako yote!
4. Utatimiza malengo yako siku zote
5. Utakuwa na marafiki ndani na nje ya ofisi yako.

Hasra za kufanya kazi kama kazi

1. Kutoa muda wako mwingi kwa ajili ya wengine
2.  Wale unaofanya kazi nao kukutegea kwani wanajua wewe hutakubali jahazi lizame
3. Unaweza kupoteza haki zako kutokana na kwamba wewe unachojali ni kutimiza wajibu wako na siyo malipo malipo kwako si kitu muhimu. La muhimu kwako ni kutimiza kazi yako.
Hivyo nakushauri uchukue hatua ufanye kazi kama kazi kwani hata kama watakudhulumu haki yako itapatikana au niseme utaipata tu!
Wewe wekeza kwenye jamii siku moja utalipwa hadi ushangae.
Mika Ayo - Mwalimu


No comments:

Post a Comment