Saturday, June 11, 2016

UMUHIMU WA KUFANYA UTAFITI

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo nataka nizungumze kwa kifupi juu ya utafiti na umuhimu wake kabla hujawekeza.
Utafiti utakusaidia kujua mambo kadhaa katika biashara au shughuli unayo taka kuwekeza.
Watu wengi huanzisha biashara kabla ya kujua ugumu na changamoto zilizoko kwenye biashara husika!
Watu hujiiingiza kwenye biashara eti kwa kuwa tu ndugu au rafiki yao fulani amefanikiwa kwenye biashara hiyo.
Ngoja nikupe siri moja. HAKUNA MTU ATAKAYE KUONA UKIWA CHINI NAMAANISHA KABLA YA KUFANIKIWA. Mara zote watu watakuona pale unapofanikiwa na huwa hawakumbuki umeteseka miaka mingapi au ni magumu mangapi umepitia kabla ya kufikia hapo ulipo. Wao hufikiri ni rahis kufanikiwa hivyo hukurupuka na baadaye wanapata hasara.
Ili usipate hasara ya muda na fedha na mwisho kukata tamaa na maisha ni vizuri ukafanya utafiti wa kutosha juu ya biashara yako mpya unayotaka kuanzisha.
Utafiti utakusaidia mambo yafuatayo ( haya ni machache kati ya mengi)
i) Kujua ukubwa au udogo wa soko la bidhaa zako
ii) Kujua washindani wako katika biashara na nguvu walionayo kwenye biashara husika
iii) Kujua watu wa kukusaidia ili uweze kuanza biashara husika
iv) Kuamua mchepuo (niche) wa biashara yako kwa mfano kama unataka kuanzisha biashara ya huduma ya kuhudumia watalii basi unaweza kuangalie wewe ujikite kwenye mchepuo gani kutokana na vigezo ulivyo navyo wewe
v) Kujua masuala ya kisheria yahusuyo biashara husika
vii) Kujua hitaji ambalo bado halijatoshelezwa kwenye biashara husika (hii inaweza kuwa ndiyo nguvu na nguzo muhimu sana kwako ambayo itakupa mafanikio kwani utakuwa unawasaidia watu kutatua matatizo au tatizo ambalo bado halijatatuliwa na ukiweza kutoa ufumbuzi basi umepiga BINGO)
viii) Kujua pa kuanzia na mengine mengi
Hivyo nakushauri ndugu yangu usikurupuke kuanza biashara wewe fanya utafiti kwanza ndipo uchukue maamuzi kutokana na taarifa ulizo kusanya kwenye utafiti wako.
Asanteni
Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment