Saturday, May 21, 2016

JINSI WATU TOFAUTI WALIVYO UTAFSIRI MUDA

Wapenzi wasomaji wa makala zangu. Watu wengi wametafsiri muda kwa kuhusianisha na mambo mbalimbali na jinsi tunavyoweza kuutumia muda wetu vibaya ama vizuri. Leo nitakupa hadithi ya Mwenyenzi Mungu, Binadamu, Mbwa, Punda na Nyani.
  Kama tujuavyo vitabu vya dini hasa Dini ya Kikristo na Kiisilamu zinakiri kwamba Mwanadamu na viumbe vyote viliumbwa na Mungu.
Sasa Wakati wa kuumba ilikuwa hivi: (hii ni kwa mujibu wa simulizi zangu na siyo kwa mujibu wa dini yoyote) Mweneyenzi Mungu alikusudia Binadamu aishi miaka 20 katika dunia hii. Lakini unajua kwa nini miaka ya Binadamu huwa 70 au zaidi?
Ilikuwa hivi Mungu alipomaliza kumuumba Mwanadamu akampa miaka 20 ndipo alipo muumba na Mbwa.
Mungu akampa mbwa miaka 20 ili amlinde Binadamu, basi mbwa akalalamika sana akisema " Mwenyenzi Mungu kweli kazi ulionipa ni ngumu sana hebu fikiria miaka 20 nikiwa nje jua langu, mvua yangu kukimbizana na hatari mbalimbali kwa kweli ni mateso makubwa sana" Mungu akamuuliza Mbwa sasa unataka nifanye nini Mbwa akajibu naomba unipunguzie hiyo miaka ili niishi miaka 10 tu" Mungu akakubali akaipunguza hiyo miaka 10. Binadamu akamuomba Mungua ampe hiyo miaka 10 aliyopunguza kwa Mbwa. Mungu akampa binadamu hiyo miaka hivyo ikawa ataishi miaka 30. Mungu akamuumba Punda ili aishi miaka 30 akimtumikia Mwanadamu. Punda naye akamuomba Mungu ampunguzie mika 20 ili aishi miaka 10 kwani alisema kazi ya kubeba mizigo miaka 30 ni ngumu sana. Pia Mungu akampunguzia miaka 20 akabaki na miaka 10.    Mwanadamu kuona hivyo akamuomba Mungu amongezee miaka 20 aliyopunguza kwa Punda na Mungu akakubali akamuongezea miaka 20 hivyo Binadamu akawa na miaka 50. Mungu akamuumba nyani ili afurahishe Mwanadamu kwa kurukkaruka juu ya miti na aishi miaka 30. Nyani naye kama wale wengine akaomba apunguziwe miaka kutoka 30 hadi 10 kwani pia aliona kuwa miaka 30 itakuwa mateso makubwa sana. Mungu akakubali na kama kawaida ya Binadamu akaomba aongezewe hiyo miaka 20 aliyopunguziwa nyani.
Mungu akampa Binadamu hiyo miaka 20 aliyoipunguza kutoka kwa nyani.

MATOKEO YAKE NDIYO HAYA
Miaka 20 Binadamu huishi maisha ya raha sana analishwa, anavishwa anasomeshwa bure akiugua anatibiwa na wazazi au walezi.
Miaka 10 ya Mbwa - (yaani 21-30) anaishi maisha ya Mbwa hasa mbwa koko. Hana ratiba ya kula hajuhi atalala wapi siku hiyo, analinda mchumba, analinda jamii yake yaani ni mahangaiko makubwa sana.
Miaka 20 ya Punda (yaani 31-50) anageuka punda wa kubeba mizigo. Atabeba mizigo ya familia, atabeba mizigo ya jamii kama kiongozi wa ngazi fulani. Na hakuna kupumzika katika kipindi hiki.
Miaka 20 ya nyani (yaani 51-7+) anageuka nyani jinsi anavyotembea ni kama nyani, pia sura inabadilika inafanana na nyani hasa usoni. Hivyo anageuka kituko na wajukuu wanaanza kumcheka.
Wewe je, uko hatua gani?
Mimi niko kwenye ile hatua ya 51+ na kwa uzoefu wangu watu wengi wanapofikia umri huu hujuta na kuikumbuka ile miaka ya Mbwa na Punda jinsi walivyoitumia vibaya.
Nakushauri hebu panga muda wako vizuri ili usije ukajuta hapo baadaye.
Nikutakie siku njema

Mika Ayo _ Mwalimu 

No comments:

Post a Comment