Thursday, May 12, 2016

JINSI YA KUJIPATIA KIPATO KWA NJIA NNE TOFAUTI

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Mara nyingi kuna mbinu rahisi sana za kutengeneza fedha na wakati mwingine huwa tunazi tumia na pengine kuna nyingine ambazo ni nzuri zaidi lakini hatuzitumii.
Ni matumaini yangu kuwa utasoma makala hii na baada ya kuisoma utachukua hatua stahiki ili uweze kupata faida.

1. Kipato cha kuajiriwa au kujiajiri
Kipato hiki ni kipato ambacho watu wengi hapa Tanzania na duniani kwa ujumla tunakifahamu sana na kukitumia. Kipato hiki hupatikana kwa kuuza ujuzi wetu, kuuza bidhaa zetu au kutoa huduma yoyote ambayo tuna ujuzi nayo.
Katika kipato cha aina hii malipo huwa ni kwa saa, wiki au mwezi kutegemeana na hali na aina ya kazi na mkataba wa mwajiriwa. Aidha watu wengi sana husoma na kujifunza mambo mapya kila siku ili waweze kunufaika kwenye ajira zinazopatikana kwenye aina hii ya kipato. Aina hii ya kipato ni ya msingi sana kila mtu kuwa nayo lakini si vyema kubaki kwenye aina hii tu ni vizuri ukaingia pia kwenye aina nyingine ya kipato.

2. Kipato kutoka riba ya pesa zako
Hii ni aina nyingine ya kipato ambapo unaweka pesa benki ili ikuzalishie hela kwa njia ya riba. Mabenki mengi hapa nchini hutoa huduma hii kwa mtindo wa huduma ijulikanayo kama akaunti ya muda maalum. Katika aina hii ya kipato muda hutofautiana kati ya miezi mitatu hadi miezi 36 au miaka mitatu. Riba utakayopata inategemea mambo makuu mawili i) Muda - kwa kadri utakavyoweka kwa muda mrefu zaidi riba au kiasi cha fedha utakayolipwa kitaopngezeka. ii) Kiasi cha fedha utakayo weka kama ni kikubwa basi na riba huwa kubwa vile vile.
Uzuri wa aina hii ya kipato ni kwamba wewe ukishaweka pesa yako benki kwa mtindo huu unaendelea na maisha yako. Ni kazi ya benki kuhakikisha kuwa pesa hii inazalisha na wewe unapata faida kama ilivyo kwenye mkataba. 

3.  Kipato kutokana na umiliki wa hisa kwenye kampuni
Njia hii hukupatia kipato pale ambapo wewe unamiliki sehemu ya kampuni fulani kwa njia ya kununua hisa za kampuni husika. Mara nyingi kampuni kama hizi hutoa gawio la faida mara moja au mbili kwa wanahisa wake. Kwa hapa Tanzania kama unataka kunufaika na njia hii ya kipato basi unaweza kuwasiliana na soko la hisa la Dar es salaam angalia website yao. www.dse.co.tz kwa maelezo zaidi

4. Kuongezeka Mtaji (Capital Gain)
Njia hii hutokana na wewe kununua nyumba au shamba au kiwanja kwa bei fulani kwa mfano unaweza kununua kwa shilingi 10,000,000 na baada ya miezi sita kiwanja au nyumba hiyo ukaiuza kwa shilingi 15,000,000 inamaana hiyo shilingi 5,000,000 ndiyo ongezeko lako la mtaji (capital gain).
Ni vizuri ukajifunza kutumia njia zote au angalau mbili katika kujipatia kipato. Kwani kubaki kwenye ile njia ya kwanza tu itakuletea matatizo ya ukosefu wa fedha baadaye.
Ni matumaini yangu kuwa utachukua hatua.
Ni Mimi
Mika Ayo - Mwalimu
Mawasiliano 0673506836
asante

No comments:

Post a Comment