Monday, May 30, 2016

JINSI YA KUWAPATA WATU WENGI

Habari za leo ndugu wasomaji wa makala zangu.
Leo nataka kujadili kwa kifupi jinsi ya kuwapata watu wengi zaidi katika biashara yako au kanisa lako au kazi yako.
Kabla sijazungumzia mbinu hizi ni muhimu kujua kuwa mafanikio yetu yanatokana na idadi ya watu tulionao.
Hakuna kazi au shuguli au biashara inayoweza kufanikiwa ikiwa haina watu wa kutosha wanaoiunga mkono!
Ili kuwapta watu tufanye nini?

1. Tuwapende watu
Upendo ni kitu hadimu sana katika maisha ya dunia ya leo. Mara nyingi watu wamekua wakiwatafuta watu wajiunge kwenye biashara zao ili wawafaidi na sio ili wale watu wapate faida itokanayo na bidhaa au huduma wanayo toa. Kama tunawatafuta watu ili tuwafaidi hapa kunakuwa hakuna upendo. Pia tujue kuwa badala ya kujijengea marafiki tunaongeza maadui jambo ambalo halitakiwi kabisa.
Kama tunawapenda watu tutawaonyesha jinsi ambavyo, huduma au bidhaa zetu zinavyoweza kuwabadilisha maisha yao yakawa bora zaidi (ni muhimu kuhakikisha kuwa tunacho waambia ndivyo kilivyo). Kwa kufanya hivyo watu wengi watakuja upande wetu na kutupa kile tunacho taka kwani sisi pia tumewapa wanacho taka. Hii ni kanuni ya maisha.

2. Kufanya ufuatiliaji
Mara chache sana huwa tunafanya ufuatiliaji wa matokeo ya huduma au bidhaa tulio uza ilivyo msaidia au kutomsaidia mteja. Jambo hili ni baya sana kwani kama kuna mteja ambaye alipewa maelezo yasiyo sahihi juu ya namna ya kutumia huduma au bidhaa yetu akaitumia ndivyo sivyo basi mtu huyo atakuwa balozi mbaya kwa upande wa biashara yetu. Lakini kama tunafanya ufuatiliaji itakuwa rahisi kugundua na kufanya marekebisho. Unaweza kutumia njia mbali mbali za kufanya ufuatiliaji ikiwemo kuweka sunduku la maoni, kuandaa hojaji fupi la kuwauliza wateja wako wa mara kwa mara ili kujua wanavyo ridhika au kutoridhika na huduma unayo toa. Kitendo cha kufanya ufuatiliaji huwafanya watu waone kuwa wanajaliwa, wanathaminiwa na wanapendwa hata kama kulikuwa na kasoro iliyojitokeza basi watu huwa tayari kuisahau na kuendelea mbele.

3. Kutoa Motisha
Binadamu alivyo umbwa anapenda sana kupongezwa. Wala mtu yeyote asikudanganye eti kuwa yeye hapendi kupongezwa. Kila mtu anapenda kupongezwa. Ni vizuri kuwapongeza watu walio kuja kutaka huduma kwako. Pongezi ya mdomo tu wakati mwingine inatosha. mfano; karibu tena, asante kwa kututembelea (wapongeze hata kama hawajanunua kitu).

4. Uvumilivu

Ni muhimu sana kuwavumilia watu hata kama wakati mwingine wamekukosea. Usitake kugombana nao tafuta njia muafaka ya kuachana nao kwa amani. Kwani hujui kama mtu huyu ambaye unakuwa adui naye huenda kesho akawa mahali ambapo unahitaji msaada kutoka kwake.

Ndugu Msomaji kwa leo niishie hapa. Nakutakia mafanikio mema kwenye maisha yako.

Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment