Monday, July 18, 2016

SIRI Iko Kwenye Kung'ang'ania

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo nataka nizungumzie jinsi ilivyo muhimu kung'ang'ania unapo anza kufanya jambo unaamini kuwa litaleta mabadiliko katika jamii yako na wewe mwenyewe mtapata mafanikio kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
Kuto ng'ang'ania kunaweza kukupa hasara kubwa kwenye maisha yako.
Hapa ngoja nikupe mifano hai miwili ya watu ambao waliwekeza nguvu sana kwenye jambo na walipo karibia mafanikio wakaacha na wenzao wakaanzia pale walipoachia na kwa muda mfupi sana wakapata mafanikio makubwa.
1. Ugunduzi wa kinywaji cha 7Up
Mtu aliye anza kufikiri kutengeneza soda nzuri ya tofauti alianza kwa kufanya utafiti na soda hiyo akaita 1UP, haikufanikiwa akaendelea akatengeneza 2 UP nayo pia haikufanya vizuri sokoni. Akaendelea kuboresha akaja na 3Up ambayo pia ilimwangusha. Kwa kifupi akaendelea na utafiti na alipofikia 5Up akakata tamaa. Baada ya kama miaka miwili kupita mwenzake akachukua ile kazi yake akajifunza makosa yaliyopo akayarekebisha akaja na 7UP ambayo ilifanya vizuri hadi leo.
Kwa kifupi kama yule aliye anza kutafuta kinywaji cha  7Up ange ng'ang'ania angepata mafanikio lakini akakata tamaa.

2. Mchimbaji wa dhahabu aliye acha kazi wakati imebaki futi moja tu kufikia dhahabu
Mfano mwingine ni wa Bwana mmoja ambaye aliamua kuchimba dhahabu hivyo akaanza kazi hiyo. Kama ujuavyo kazi ya uchimbaji wa madini ni ngumu na ya gharama kubwa sana! Huyu mtu alichimba kwa muda mrefu mwisho akachoka akakata tamaa. Kwa kuwa lile eneo alilolitumia kwa uchimbaji alikuwa analimiliki kisheria basi aliamua kuuza kwa mtu ambaye anataka kuchimba dhahabu. Mtu mmoja akaamua kulinunua lile eneo. Baada ya kulinunua akamwaajiri mtaalam wa miamba ili afanye uchunguzi. Yule mtaalam akagundua kuwa wakati wa uchimbaji wale waliokuwa wakichimba walipoteza njia walipokaribia dhahabu na akafanya marekebisho madogo ambapo walipochimba kiasi cha futi moja yaani sentimenta 30 tu akawa amepata dhahabu! Yule mmiliki wa awali aliposikia alijuta sana. Ingawa hakurudi tena kwenye uchimbaji wa dhahabu alijikita kwenye kazi yake mpya ya uuzaji wa Mikataba ya bima ambapo aliamua kutokata tamaa tena.

Hivyo nakishauri kama kunakitu unafanya usikate tamaa wala usiangalie wala kusikiliza maneno ya watu. Watu wengi wata kukatisha tamaa au watakuondoa kwenye lengo lako ili wakufanye wewe uwe chambo ili wafikie malengo yao baadaye wakucheke. Na kadhalika hivyo NG'ANG'ANIA WALA USIACHE UNACHOKIFANYA.

Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment