Wapendwa wasomaji wa makala zangu.
Karibuni sana kwenye
darasa letu hili la kujikwamua kimaisha.
Leo nimeamua tuzungumzie suala la jinsi ya kuwapata
marafiki, hasa watu wageni au watu ambao tungependa kuwafahamu au watufahamu
kutokana na umuhimu wao kwetu na kile tunachokifanya au tunachotarajia
kukifanya. Mara nyingi watu hushindwa kuanza au kuanzisha mazungumzo na watu
kwa njia sahihi na mwisho huishia kuwapoteza watu ambao wangekuwa muhimu sana
kwenye maisha yao.
Hivyo kama ungependa kupata mbinu hizi karibu usome makala
hii. Mbinu hizi zitakusaoidia si, tu kupata marafiki lakini pia itakusaidia
kupata wateja wapya katika biashara yako.
JINSI YA KUFANYA
1. Unaweza kukutana na mtu kwenye basi au hospitalini au mahali popote. Kwanza msalimie na ujitambulishe jina lako na
kumuomba akuambie jina lake. Akisha jitambulisha nenda hatua ya pili ya
mazungumzo yenu.
2.
Mwambie habari ya Familia yako. Mfano mimi
nimeoa na nina watoto watatu wawili na mdogo wa mwisho ni wa kiume. Vipi wewe
mwenzangu? Ataanza kukueleza kuhusu familia yake na kama hapendelei sana kuhusu
kueleza mambo ya familia basi unaweza kukatisha sehemu ya mazungumzo kwa
kuendelea sehemu ya tatu ya mazungumzo yenu ambayoni :
3.
Kumjulisha kazi au biashara unayoifanya na
kumtaka yeye naye akueleze juu ya kile anachokifanya. Akisha kukueleza jitahidi sana kusifia kitu
kutoka yale aliyo kueleza. Kwa mfano kama amekuambia yeye ni daktari wa
binadamu basi mwambie ah! kazi yako ni nzuri sana, naamini kati ya watu
wanaofanya wajibu nyeti na muhimu ni madaktari. Au kama ni mfanyabiashara basi
sifia kwa vyovyote kile wanachokifanya.
Kwa kufanya hivyo utamsogeza karibu zaidi
na wewe kwani ataona kuwa amethaminiwa sana.
Kufikia hapo mtakua mmesha anzisha
mahusiano na kama umecheza karata yako vizuri mtakuwa mmeshapeana namba za simu
na kupeana miadi ya siku nyingine ya kukutana ili mwendeleze mazungumzo yenu.
Pia kama una biashara yako ambayo ungetaka kumshirikisha/ kumuuzia basi mtakuwa
mmeshakubaliana jinsi ya kuifanya katika hatua za awali. Kama kufikia hapa bado
hujampata kwa maana ya kumshirikisha biashara yako basi nenda kwenye hatua ya
nne nay a tano kama ifuatavyo:
4.
Burudani
Kuna baadhi ya watu ambao katika kuongea
nao wao hawafurahi sana wakisikia neno BIASHARA kwani wao hujiona kuwa sio
wafanyabiashara ingawa kwa namna moja ama nyingine kila mtu ni mfanyabiashara.
Ila wao hupenda baadhi ya burdani, kama vile mziki, mpira wa miguu, pool table
na kadhalika. Ukiona anahamasika kwenye
hatua hii basi angalia jinsi ambavyo kile unachokifanya (biashara yako) inaweza
kumsaidia katika kufanikisha burdani yake ikamfaa zaidi. Kama biashara yako
haiingii hapo usilazimishe mambo ishia hapo tu kwa kumpata rafiki kwani huenda
siku moja atakufaa katika jambo jingine. Lakini ukiona bado hujampata ili aweze
kuwa mteja au kujiunga ili mfanye biashara kwa pamoja nenda hatua ya mwisho ya
tano:
5.
Hamasa
Watu tofauti huamasishwa na mambo tofauti
tofauti ingawa watu wengi sana huamasishwa na kupata kipato cha ziada kwa maana
ya ‘PESA’. Kama ukishajua kuwa huyu mtu
anahamasishwa na nini basi mweleze/ muonyeshe jinsi biashara yako inavyoweza
kujibu swali lake/hamasa yake.
Watu wengine huamasishwa na kutoa huduma
kwa jamii.
Fuata pia kanuni hizi unapo zungumza na
watu:
·
Tabasamu – tabasamu husaidia sana kumuondolea
unayezungumza naye hofu au wasiwasi kwani siku hizi kuna matapeli wengi. Ila
kama utakuwa na tabasam la bashasha basi husaidia mwenzako kujenga kukuamini na
kuwa karibu zaidi na wewe.
·
Usiulize maswali kama ya polisi – acha muda
upite kidogo mpe msikilizaji wako muda kidogo wa kutafakari uliomuuliza
usiongee kama cherehani pia msikilize na mwache aulize maswali ili ajenge kukuamini. Ingawa unatakiwa kuwa mwangalifu katika sehemu hii ya maswali hakikisha wewe ndiye unaye uliza zaidi katika hatua za awali.
·
Ukiona mtu hataki kukusikiliza usilazimishe,
jaribu kuanzisha mazungumzo na mtu aliyeko jirani yenu na yule mtu akikuelewa
unaweza kushangaa kupitia jirani yenu yule uliyetaka kuzungumza naye anajileta
mwenyewe kutokana na mazungumzo mazuri anayo yasikia kutoka kwa wewe na jirani
yenu.
Kumbuka binadamu amafundishwa
tangu akiwa mdogo kufanya au kutoa kitu anapo ombwa ndiyo maana ukiulizwa jina
utasema jina lako. Ukiulizwa njia ya kuelekea eneo unalolijua na mgeni unatoa
msaada nakadhalika.
Ukitaka kujua zaidi juu ya hili
soma makala yangu inayozungumzia : JINSI YA KUPATA CHOCHOTE UNACHO TAKA.
Nakutakia kila la kheri katika
kukuza idadi ya marafiki kwa kutumia mbinu hizo hapo juu, na nyingine ili
uongeze idadi ya marafiki zako na idadi ya wateja wako na idadi ya watu
watakaokusaidia kwenye bisashara yako.
Asanteni sana
Mika Ayo.
No comments:
Post a Comment