Ndugu wasomaji wa blog yangu karibuni tena ili tushirikishane
maarifa juu ya jinsi ya kufanikiwa na kupata ‘PESA’ na mafanikio mengine.
Jinsi ya kufanikiwa
1.
Ili uweze kufanikiwa ni lazima ujue
unachokitaka.
Mara nyingi watu huangaika katika maisha na
ukiwaona utadhani kuwa wamefanikiwa sana, kumbe! Baada ya muda hawana kitu au
kama wanacho; hawana raha! Kwa nini? Ni kwa sababu hawajuhi wanachokitaka katika
maisha yao.
Ni vigumu sana kupata furaha katika dunia
hii kama hatujuhi tunachokitaka. Tatizo kubwa huanzia nyumbani katika familia
zetu. Katika familia zetu za Kiafrika ni rahisi sana kumfundisha mtoto adabu na
utii kwa wakubwa na wadogo. Na mara nyingi mtoto anatakiwa kusikiliza
anachosema mkubwa lakini yeye siyo rahisi kusikilizwa! Jambo hili limeharibu na
kuathiri watu wengi wanapokuwa watu wazima kwani hawakupewa ile haki ya msingi
ya kuamua ni nini wanachotaka katika maisha yao, hata pale mtoto anapokuwa yuko
sahihi. Mara nyingi wazazi wanapandikiza kile wanachotaka ndani ya watoto wao.
Watoto wanapo kuwa watu wazima wanajikuta wanaendesha maisha kwa kufuata mzazi
anataka nini, ni kama kufukuza upepo
Hawajui watokako wala waendako, hawana mwelekeo, hawana furaha, wamekata tamaa!
Hawajui wanataka nini katika maisha kutokana na kukosea toka awali kwenye
makuzi yao.
Hawajui watokako
wala waendako, hawana mwelekeo, hawana furaha, wamekata tamaa! Hawajui
wanataka nini katika maisha kutokana na kukosea toka awali kwenye makuzi
yao.
|
Ni lazima ujiulize kuwa je, hivi mimi
nataka nini katika maisha yangu? Nataka nini kitokee katika maisha yangu leo,
wiki hii, mwezi huu, mwaka huu na kadhalika ili niweze baadaye kupata kile
ninachokitaka.
Kama hujuhi unachotaka katika maisha yako
ni vigumu sana kujua unapo kipata, unaweza ukajenga nyumba usio itaka kwa kuwa
tu kila mtu anajenga nyumba na wewe unayo pesa na utajenga na utaishi ndani
yake lakini utashangaa huna furaha! Kwa nini ni kwa sababu sicho ulicho kihitaji. Utaoa, utasoma,
utafanya kila kitu lakini hutapata furaha kwa nini; kwa sababu hujuhi
unachokitaka.
Njia pekee ya kujua unacho kitaka ambacho
kitakupa furaha katika maisha yako ni kutafuta unacho kitaka!
Njia pekee ya kujua unacho kitaka
ambacho kitakupa furaha katika maisha yako ni kutafuta unacho kitaka!
|
Kitabu cha Biblia kinatufundisha
jambo hili vizuri “….tafuteni nanyi mtaona” Luka sura 11 mstari 9 (Luka 11:9) hapo juu nimeeleza juu ya wazazi
wanavyoweza kutupotosha juu ya yale tunayoyataka(hapa ifahamike kuwa
nazungumzia mambo makubwa katika maisha yetu). Wazazi wanayo sehemu muhimu sana
katika kuyaandaa makuzi ya watoto wao kulingana na mahitaji ya jamii wanayo
ishi. Ila mimi naona kuwa ni kosa kwa mzazi kumwiingilia mtoto katika maisha
yake ya baadaye. Mfano mzuri ni kwamba mzazi anaweza kumchagulia mtoto kazi
atakayo ifanya katika jamii atakapo kuwa mtu mzima. Kutokana na malezi na makuzi mtoto naweza
akachukua mwelekeo alio ambiwa na mzazi lakini akawa hana furaha kabisa. Pia
hofu katika maisha inaweza kutusababisha tukajiingiza kwenye fani ambazo
hatuzipendi. Mfano mzuri ni kipindi hiki cha uhaba wa ajira vijana wengi
wanajikuta wanaingia kwenye fani ili tu kupata ajira “PESA” lakini hawapendi kabisa fani husika. Katika
hali kama hii ni vigumu sana kufikia malengo kwani tunajikuta tunafanya jambo
tusilolipenda. Ni muhimu tufanye jambo tunalolipenda na kupitia jambo hilo ni
rahisi sana kufanikiwa.
Sasa kwa wale ambao bado hamjajua
mnachokitaka katika maisha yenu basi hii ni fursa kwenu kuchukua hatua kutafuta
kile ambacho mnakitaka katika maisha yenu. Kwa kiingereza wanaita “Soul
searching” hii ni kama unafanya kazi ya kuihoji nafsi yako juu ya jambo hilo.
Unaweza kujiuliza maswali yafuatayo:
i)
Je, mimi ni mzuri katika Nyanja zipi? (kuimba,
kuchora, nina uwezo kuhamasisha watu
wakafanya nitakalo, nina uwezo wa kuigiza n.k)
ii)
Je, nikifanya jambo hili Napata furaha?
iii)
Je, katika jambo hili naweza kuona mafanikio
ndani yake miaka mitano kumi ijayo?
iv)
Ni nani wanaweza kunisaidia (mentors)
Jambo hili siyo rahisi sana ila tu nakuhakikishia linawezekana.
Unalifanya wewe mwenyewe kwa
kujihoji, kusoma vitabu, kuwauliza watu wengine na kadhalika.
Kwanza nikupe hongera kama umeweza
kusoma makala hii hadi kufikia hatua hii basi wewe uko juu ya watu 90% hapa
duniani hivyo nakuhakikishia ukiendelea na tabia hii ya kusoma machapisho kama
haya na vitabu vingine na hasa ukayaweka
katika vitendo mambo unayojifunza utafanikiwa sana katika maisha yako kipesa na
maongezeko mengine mengi.
2. Kanuni
ya pili ni “KUOMBA” au “KUULIZA”
Neno hili kuomba
kwenye Biblia ya Kiingereza limeandikwa “ask”
ambapo kwa tafsiri ya kawaida ya Kiswahili ni kuuliza. Lakini kwa kweli
ili wewe msomaji wa makala hii uweze kupata ile faida ninayotaka uipate basi
nitakuwa natumia maneno haya yote mawili kulingana na haja itakayo jitokeza.
Watu wengi
ukiwauliza kwa nini hawajaanzisha biasha ambazo wana ujuzi wa kuzifanya
watakuambia ni kwa sababu hawana mtaji.
Watu wengi
wanafikiri kuwa ‘PESA’ ndicho kikwazo
kikubwa cha wao kutofanya yale ambayo wanataka kuyafanya kumbe siyo kabisa!
Watu wengi wanafikiri kuwa
‘PESA’ ndicho kikwazo kikubwa cha wao kutofanya yale ambayo wanataka
kuyafanya kumbe siyo kabisa!
|
Tatizo linaweza kuwa ni wewe
kutokuuliza (kufanya utafiti) kile unacho takiwa kukifanya. Hebu nenda kaulize
kwa watu waliofanikiwa kwenye jambo unalotaka kulifanya, utashangaa utakavyo
weza kupata msaada wa mawazo na hata pesa za kukusaidia kufanya kile
unachotaka.
Usishangae nikikuambia kuwa
unaweza kupata pesa kwa kuuliza. Unapo uliza Yule unaye muuliza anayasikiliza pia mawazo yako na akiona kuwa unalo
wazo lenye tija yuko tayari kuwekeza kwenye wazo lako! Kwa nini anataka kupata
“PESA” na kumbuka kuwa mwenye wazo ni wewe hivyo hana jinsi ya kukuacha lazima
akushike mkono ili umongoze katika wazo lako mpate pesa. USIOGOPE ULIZA.
Kuomba pia kunaweza kukutoa kwenye
lindi la umasikini. Naomba unielewe hapa kuwa simaanishi kukufanya uwe omba
omba au Matonya. Ninacho maanisha ni kuwa nakufundisha saikolojia ya watu!
Binadamu tangu akiwa mtoto amefundishwa kutoa anapoombwa au kujibu
anapo ulizwa!
Binadamu tangu akiwa mtoto amefundishwa kutoa anapoombwa au kujibu
anapo ulizwa! Usiipoteze nafasi hii ya wazi namna hii itumie utaona maisha
yako yanaanza kubadilika!
|
Kwa mfano, kama unataka kuanzisha
biashara katika eneo fulani (wewe furaha yako ni kutoa huduma kwa wateja wako
kwa bei nafuu na kukidhi mahitaji ya watu/wateja) katika mji wako na shida yako ni pesa ya
kupanga chumba cha biashara. Hebu kaa na fikiria kidogo fanya utafiti kama kuna
eneo au chumba ambacho kipo wazi ambacho unaweza kukitumia kwa biashara yako.
Fikiri jinsi ambavyo kwa kufungua biashara yako mwenye nyumba anaweza kunufaika
(pamoja na kwamba hutamlipa kodi) muombe ukitumie kwa muda mweleze hali halisi.
Kwa kuwa bianadamu amefundishwa tangu utoto kutoa jibu lazima utafanikiwa.
Nakuhakikishia hata kama mtu wa kwaza na wa pili atakataa lakini kuna mmoja
atakukubalia. Kwa nini hii ni moja ya Kanuni za maisha kama ilivyo kanuni
mbalimbali za kisayansi zinavyofanyakazi hii nayo inafanya kazi vilevile.
OMBA/ULIZA
Nenda ukaifanyie kazi mambo
uliojifunza hapa una subiri nini ondoka ….. fuata mafanikio> yako.
Asante.
No comments:
Post a Comment