Wednesday, March 30, 2016

Jinsi Ya Kuandika Barua ya Kuomba Mkopo Benki

“People who ask confidently get more than those who are hesitant and uncertain. When you've figured out what you want to ask for, do it with certainty, boldness and confidence. Don't be shy or feel intimidated by the experience. You may face some unexpected criticism, but be prepared for it with confidence.” ― Jack Canfield Ndugu wasomaji wa makala zangu. Habari za leo. Naomba leo nitoe changamoto ya Jinsi ya Kuandika barua ya maombi ya mkopo. Hii naita changamoto kwani kuna njia mbali mbali za kuandika barua za namna hii. Baadhi ya vyombo vya fedha hutoa fomu ambayo inakuongoza hatua kwa hatua mambo ya kujaza na ukisha jaza basi unakua umesha eleza mambo yote yanayotakiwa. Lengo la mada hii ni kuchokoza fikra za ubunifu wa “wewe” au “sisi” wenyewe kuwa ndio chanzo cha kuanzisha wazo la kuomba mikopo kutoka kwenye vyombo mbalimbali vya fedha vilivyopo katiak maeneo yetu. Nitapenda sana kama nitasikia kutoka kwenu kama kuna mtu ambaye ameweza kuandika barua yake ya kuomba mkopo na mkopo ukakubaliwa. Kama taniruhusu nitaiweka wazi kulingana na matakwa yake. Nikiwa na maana kama atataka tutumie majina yake halisi ama la, basi tutafanya hivyo hivyo kulingana na matakwa yake lengo ni kujifunza. Basi leo sitaki kuchukua mud asana nakala ya barua iko hapo ukurasa unaofuata. Mika Ayo- Mwalimu Asanteni MIRISHO MASAI ALEI S.L.P 7443, ARUSHA 23/09/2015 MENEJA MKUU, BENKI YA WANANCHI WETU, S.L.P 20,000 USA RIVER, ARUSHA YAH: MAOMBI YA MKOPO WA TZS 3,410,800 KWA AJILI YA KUENDELEZA MRADI WA UFUGAJI WA SUNGURA. Husika na somo la hapo juu, Mimi ni mkazi wa mjini Arusha Kata ya Muriet. Kwa jina ni Mirisho Masai Alei kama ilivyo kwenye anuani hapo juu. Mimi ni Mteja wa Benki yenu mwenye akaunti namba 002 inayojulikana kwa jina la Mirisho Masai Alei ambayo ndiyo nitakayoitumia kupokelea mkopo na baadaye kulipia mkopo wangu pindi utakapo kubalika na kupitishwa. Kusudi la barua hii ni kuomba mkopo wa shilingi 3,410,800/ (milioni tatu na laki nne na elfu kumi na mianane tu) kwa ajili ya kukuza mradi wangu wa ufugaji wa sungura. Mradi kwa sasa umeshaanza na wana idadi ya sungura wapatao 14. Kati ya hao majike ni 10 na dume ni 4. Sungura hao majike 10 watatumika katika kuzalisha watoto kwa ajili ya kuuza sokoni kama ilivyoelezwa kwenye barua hii hapochini. Mradi wote utagharimu kiasi cha shilingi 4,643,800/ (milioni nne laki sita arobaini na tatu elfu na mia nane tu). Kiasi kinachoombwa benki ni sawa na asilimia 73.45 ya mradi wote na muombaji atatoa asilimia 26.55 ya gharama yote ya mradi. Dhamana ya mkopo ni kiwanja changu kilichoko kwenye eneo la Lolovono chenye ukubwa wa mita 14 x 22 chenye thamani ya shilingi 6,000,000/ (milioni sita) katika eneo ambalo halijapimwa. Nakala ya hati pamoja na barua ya mtendaji wa Kata vimeambatanishwa na barua hii kuthibitisha uhalali wa umiliki. Matarajio kutokana na utaalam wa ufugaji wa sungura ni kwamba uzalishaji utaanza baada ya miezi sita tangu mradi kuanza. Aidha mradi unatarajiwa kuzalisha faida ya shilingi 400,000 kwa mwezi, kama Benki itakubali kuanza kupokea malipo ya mkopo huu kidogo kidogo, kwa maneno mengine fedha yote ya faida ni wazi kwamba mkopo huu utakuwa tayari umeshalipwa baada ya mwaka mmoja baada ya mradi kuanza uzalishaji. Hii ni sawa na kusema kuwa mkopo utaisha kulipwa baada ya miezi 18 tangu ulipotolewa. Soko la sungura nina mkataba wa kisheria na Kampuni ya Positive Eye kwa miaka sita wa kisheria wa kuwauzia sungura. Nakala ya mkataba wa uhakika wa kuuza sungura umeambatanishwa hapa. Ni matumaini yangu kuwa ombi langu litakubaliwa , Asante. Mirisho Masai Alei.

No comments:

Post a Comment