Sunday, April 17, 2016

JINSI UOGA UNAVYO KUZUIA

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Wataalamu wa mambo ya saikolojia wanatuambia kuwa kuna nguvu nyingi ambazo zimetukalia.
1. NGUVU YA MAPENZI
2. NGUVU YA HASIRA
3. NGUVU YA UOGA
Ziko na nyingine nyingi ila hizi NGUVU zikitumika vibaya huweza kutuumiza. Pia zikitumika vizuri zinaweza kutusaidia.
Mfano mmoja ni NGUVU ya uoga!
Unaogopa kuibiwa unajikinga kwa sijuhi kuweka ukuta, kengele, mlinzi, mbwa sijui nini tena?
Unaogopa kuachwa na mpenzi wako hivyo unafanya kila liwezekanalo ili hilo lisitokee.
Unaogopa kuanza biashara mpya kwa kuwa unaogopa kupoteza fedha zako lakini kubwa kuliko ni kuogopa kuchekwa na unasema kama nikishindwa je, watasemaje na kadhalika.
Hebu acha kuogopa kwani ni mangapi umeogopa na hayajakupata?
Nakupa shauri acha UOGA nenda kafanye kile ambacho moyo wako unakutuma kufanya. Nenda leo usingoje kesho. Kesho huwa ni ya Nyani yeye husema kesho nitajenga halafu kikipambazuka anakimbia kutafuta matunda na kuiba mahindi na matunda mengine kwenye shamba la binadamu, akihamaki kumekuchwa! Hana muda wa kujenga siku imekwisha anajipa tena moyo ah; kesho. Na amekuwa akifanya hivyo hadi anakuwa mzee na hatimaye anakufa.
Acha kuwa nyani ishi kama binadamu. Anza kitu kipya leo iliufurahie maisha.
Mika Ayo- Mwalimu
+255-763-506-835 mikahezekiel@hotmail.com

No comments:

Post a Comment