Wednesday, April 6, 2016

JINSI YA KUPATA MAWAZO MAPYA

Habari za leo wapenzi wasomaji wa makala zangu. Leo nataka tuangalie jinsi ya kupata mawazo mapya kwa ajili ya kubadilisha dunia yetu. Mara nyingi watu hupenda watu wenye ubunifu na watu kama hawa utaona ni rahisi kupewa kazi, kupanda vyeo kazini, kupata nafasi za kisiasa na mengine mengi. Wakati mwingine unaweza kutamani kuwa kama wao au kupata kujua mbinu wanazo tumia ili kupata mafanikio. Leo nimeamu kukushirikisha moja ya mbinu wanazo tumia ili kufanikiwa ambapo mbinu hiyo ni "MAWAZO AU WAZO JIPYA" mara nyingi mwanadamu huamasika zaidi anapoona mbinu mpya zinatumika katika kufikia malengo. Jinsi ya kufanya ili kuweza kupata wazo jipya ni kuhakikisha kuwa una kalamu na karatasi halafu anza kuandika chochote kinacho kuja kwenye akili yako "CHOCHOTE" hata kama unaona kama ni wazo la kijinga namna gani wewe liandike tu! Mtu mmoja akizungumzia jambo hili alisema kuwa mwaandishi mmoja maarufu angeweza kuanza kutafuta wazo jipya la kuandika kwa kuanzia popote. Kuna siku alianza hivi "Mwezi umetengenezwa kutokana na jibini ya kijani" Baadaye aliendelea kuandika juu ya mwezi, tena akaandika juu ya jibini na mwisho akaandika juu ya rangi ya kijani! Unaona? Ni rahisi tu. Wewe andika chochote kinachokuja halafu utaboresha baadae. Kumbuka wazo lako ni kama jiwe au tofali moja katika ujenzi wa nyumba na siyo nyumba nzima! Bado utahitaji tofali na vifaa zaidi ili kukamilisha ujenzi wa mradi wako au wazo lako ili liwe kitu kamili. Mara ukipata wazo jipya liandike haraka la sivyo utasahau, halafu endelea tena kufikiri zaidi 1) Fikiri 2) Andika 3) Zungumza mawazo yako kwa watu usiogope kuchekwa. Ukifanya hivyo kila siku utashangaa kila siku utakuwa na mawazo mapya na watu watakuwa wanakuja kwako kuomba ushauri tena siyo watu wa kawaida watakuja Matajiri, Wasomi, Wanasiasa na watu mashuhuri sana hata kuliko wewe kutaka mawazo kutoka kwako. Anza leo usilaze damu changamka. Asante Mika Ayo _ Mwalimu

No comments:

Post a Comment