Tuesday, April 12, 2016

KILA SIKU NA KILA WAKATI NI VITA

Habari za leo wasomaji wa makala zangu. Leo nataka kuwajulisha jambo moja tu. Kila siku na kila wakati ni vita. Ukitaka kwenda mjini lazima ufanye vita na mwili wako uulazimishe kuamka kitandani, uulazimishe kuchukua mswaki, uulazimishe kuoga. Utatakiwa uulazimishe kuvaa nguo na viatu. Uulazimishe kuingia kwenye gari au kwenda kwenye kituo cha dala dala. Kama haitoshi mwili hautaki kazi hivyo unayo VITA ya kuulazimisha kufanya kazi. Bosi anataka kazi aliokupangia iishe kwa wakati mwili wako hautaki! Pigana VITA ulazimishe ukae hapo kwenye kiti ufanye linalotakiwa na bosi wako. Wenyewe (Mwili wako huo) utapigana vita wa wewe, mara njaa, mara kiu mara utakukumbusha mashosti wa kuwapigia simu ili mkutane pale kwenye kijiwe chenu cha kila siku. Alimradi ni vita ili ushindwe kufikia malengo! Habari za leo Jane/James vipi leo hatuendi kupata chai ya saa nne pale mgahawani? Au ndo unajifanya mchapakazi hodari? twende bwana, ukiona hivyo hiyo ni vita kwani umepanga uachane na chai ya saa nne au basi unywee hapo kwenye dawati lako ili utimize malengo lakini kuna rafiki anafanya VITA na mafanikio yako bila yeye na wewe kujua. Usikubali. Pambana hakikisha hakuna chochote kinakutoa kwenye mstari wa kufikia mafanikio yako. Kumbuka vita viko kila mahali ndani ya mawazo yako ni vita, ndani ya familia ni vita jamii inayo kuzunguka ni vita. Hawa wote wanataka ushindwe kufikia malengo yako. USIKUBALI PAMBANA. Mwisho. Mh! Mwalimu sikuelewi eti mimi najipiga vita mwenyewe; kivipi? Ngoja nikuambie ndani yako mko wawili "WEWE" na "yeye" wewe ni Mtu wa kuwaza na kunia mambo makubwa lakini "yeye" ni mwoga mtu wa kukata tamaa na dunia nzima ni kama inamuunga mkono isipo kuwa watu wachache sana wanampinga na Kumuunga mkono "WEWE"! Sasa usipojua jinsi ya kupigana vita hivi utakuwa mtu wa kushindwa kila siku na kila kitu! Usikubali Pambana hakikisha "wewe" anamshinda "yeye" ndani yako KUMBUKA YEYE anakelele sana, mlalamikaji, mahiri sana kutoa sababu za msingi ambazo japo ni za uongo usipoangalia utaziamini na utashindwa. Tafadhali usimsikilize anavyo visingizio kibao, oh! muda hautoshi kujifunza mambo mapya kwani niko bize. Oh; siku hizi hakuna pesa ndiyo maana siwezi hata kununua kitabu cha kujifunza maarifa mapya. Oh, siku hizi maisha ni magumu na kadhalika na kadhalika. Huyo ni "yeye" Usimsikilize mpinge kwa kuchukua hatua kinyume na anavyo amini mfuate "wewe" ambaye anaamini inawezekana kupata pesa. Inawezekana kufanikiwa inawezekana kuwa TAJIRI pamoja na kwamba sasa sina chochote lakini kwa kutumia fursa zilizonizunguka na kwa kushirikiana na watu sahihi nitatoboa tu! PIGA VITA MWANANGU USISHINDWE. Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment