Monday, April 4, 2016

Sababu 10 kwa nini utafanikiwa

Wapenzi wasomaji wa makala zangu leo nataka nikuletee sababu kumi kwa nini wewe lazima utafanikiwa. 10) Dunia inakusubiri kila siku dunia inatafuta kitu cha tofauti toka mtu tofauti. Ndiyo unaweza kusema ah, mimi ni mwimbaji lakini si mwimbaji mzuri kama fulani. Ni kweli wewe si mwimbaji, au mchezaji, au mfanya biashara mzuri kama yule. Lakini wewe ni tofauti na wote na Dunia inatafuta hapana inahitaji kitu tofauti ambacho ni wewe pekee uliyenacho. Nenda Katoe hiyo huduma tofauti. 9) Kila siku kunahatua mpya unafanya au unapiga. Haijalishi kuwa ni ya kurudi nyuma au kwenda mbele. Kwa vyovyote hiyo ni hatua wala hakuna bahati mbaya. Unachotakiwa kutafakari ni kutafuta somo lililotokea kwenye jambo baya lililotokea. Je, wa jua Chanjo ya Polio iligindulika kwa bahati mbaya? mtafiti hakujua anacho kifanya katika bahati mbaya akagundua chanjo ya ugonjwa wa Polio! Hata Bara La Amerika ya Kaskazini liligunduliwa kwa bahati mbaya! Kwa hiyo usijute sana kama umepata bahati mbaya mafanikio yako kwenye hiyo bahati mbaya wewe chimba tu utaona! 8) Unao ujuzi au stadi fulani kama huna kwenye dunia hii ya utandawazi kunawatu wengi tu wako tayari kukuuzia ujuzi wao uwe mali yako kwa vijisenti na wewe utengeneze mamilioni ya pesa kwenye hiyo kazi au ujuzi wao. Unachotakiwa kufanya ni kujifunza tu juu ya namna ya kufanya hivyo! Pia kama hujui basi wako watu ambao wako tayari kukufundisha jinsi ya kufanya hivyo! 7) Uhitaji pesa ili uweze kufanikiwa! Unacho hitaji ni mambo mawili tu makubwa la kwanza ni nia ya dhati ya kutaka kufikia mafanikio, nia hiyo iwe inawaka ndani yako kiasi kwamba wakati mwingine hulali usingizi kwa ajili ya nia ya kutaka kufika kileleni. Pili ni kujua kwanini unataka mafanikio na jinsi ya kuyapata ukiwa na mambo hayo dunia yote ni mali yako! 6) Wewe si mvivu, uhitaji mtu wa kukusukuma ili uamke mapema, sio mtu wa kusukuma ili utimize wajibu wako. Ni mtu unayejisimamia mwenyewe 5) Huna wivu ukiona watu wengine wanapofanikiwa badala yake uko tayari kuwasaidia ili waweze kufanikiwa zaidi huna wivu. Unawatakia wengine mema wala huna uchungu wala siyo mtu wa kulaumu bali kila mara huwatia wengine moyo. LAZIMA NA WEWE UTAFANIKIWA KAMA WAO KWANINI? UNAKUWA KAMA SUMAKU UNAVUTA YALE YOTE MEMA KWAKO. UKIFANYA KINYUME NA HAYO UNAYAFUKUZA. 4) Wewe ni mtu unaye ishi kwa malengo kila siku unaweka lengo fulani na jioni unapima jinsi ulivyo fanikiwa kulitimiza lengo lako. Kama hukufanikiwa humlaumu mtu yeyote hata kama kwa njia moja ama nyingine amechangia katika kutofanikiwa kwako. Badala yake unaweka mikakati mipya juu ya namna bora zaidi ya kufikia malengo yako kwa kuweka mbinu za kukwepa vikwazo vilivyojitokeza ili usikwame tena katia kufikia malengo yako. 3) Kila siku unajifunza jambo jipya katika maisha yako, hususani katika biashara au kazi unayoifanya. Huchoki kujifunza 2) Wewe ni Mtafiti hufikii maamuzi bial kwanza kufanya utafiti wa kina. Hata kama taarifa utakazo tumia umepewa na watu au chanzo tofauti. Unazitumia tu kukuongoza katika kufikia maamuzi. Lakini maamuzi ya mwisho yanakuwa yako na siyo ya mtu mwingine. Uko tayari kuwajibika na matokeo ya uamuzi uliochukua kwani huo ndiyo uamuzi wako baada ya kufanya uchambuzi wa takwimu. 1) Wewe ni kiongozi unaona mbele uanaona miaka mitani kuanzia sasa. Kwa Nini unatumia historia na matukio ya siku za nyuma kuhusu kazi au biashara unayoifanya kujua ni nini kitatokea miaka mitano au kumi ijayo. Wewe unaongoza njia na wengine wanafuata. Unamaono Unahamasisha na Unahakikisha mambo yanakwenda kwa kasi inayotakiwa. Zingatia hayo kila siku na wewe utafanikiwa Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment