Thursday, April 7, 2016

JINSI YA KUJIHAKIKISHIA USHINDI

Habari za leo wasomaji wa makala zangu. Leo nataka nikupe njia pekee, na namaanisha pekee ya kujihakikishia ushindi! Kuna njia nyingi sana ambazo unaweza kuzitumia ukapata mafanikio ya kipesa au ukaondoa tatizo linalo kukabili. Lakini iko njia moja tu ambayo pamoja na kutumia njia hizo nyingine lakini hii MOJA ni ya kipekee. Unaweza Kutumia elimu yako ukapata ushindi lakini Elimu haiwezi kuzidi umahiri wa njia hii Unaweza kutumia WAZO la kibiashara ukapata mafanikio lakini hilo pia haliwzi kuizidi njia hii Unaweza kumtumia kocha (Mentor) akakuongoza lakini pia njia hiyo haitazidi njia nitakayo kuambia leo. Njia hii inaaminika na watu wote maarufu duniani kuwa ndiyo mbinu ya pekee ya kujipatia ushindi. Je, unataka kuijua? U- VU- MI-LI-VU Uvumilivu ni njia pekee ambayo itakuhakikishia mafanikio kwnye chochote unachokifanya. Ukiwa mtu wa kukata tamaa au kuzira mara changamoto zinapotokea basi jua kuwa wewe unakataa mafanikio. Kuvumilia hakuna maana ya kukaa kimya wakati mambo yanaharibika kwenye biashara au kwnye kazi yako HAPANA ila kuvumilia kuna maaana kuwa unang'ang'ania hapo huku ukitafuta suluhisho la changamoto au tatizo lililojitokeza hata kama ni kubwa kiasi gani. Kuna kisa kimoja cha jitu moja katili sana liliishi huko Marekani na jitu hilo lilikuwa halijali watu lingeweza kukupiga hata kukuua ikibidi kama ndilo linalo mpendeza, hivyo watu wakawa wanaliogopa sana. Jitu hilo lilikuwa na kiwanda na wafanyakazi. Siku moja mama mmoja aliyfanyakazi hapo kiwandani akaugua sana na akanda hospitalini. Kule hospitalini akatakiwa kulipa dola 50 ambazo hakuwa nazo! Hivyo akarudi nyumbani bila matibabu na alipofika binti yake mwenye umri wa miaka 9 akamuliza mama umepata matibabu? Mama akamjibu yule binti yake mwanangu sijatibiwa kwani daktari anahitaji dola 50 na mimi sina. Yule binti akamwambia mama, sinitume mimi kule kazini kwako nikakuchukulie hiyo hela? Mama yake akamwambia hapana kwanza ukienda huko lile jitu lenye kiwanda laweza kukudhuru usienda huko kabisa. Yule binti akamwambia mama yake mama, mimi nakwnda siwezi kuona wewe unaumwa hivi mimi nikakaa kimya lazima niende potelea mbali. Kama yule mama haja hamaki yule binti akawa ameshaondoka kuelekea iwandani alikokuwa akifanyakazi mama yake. Binti akaenda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya lile jitu. Akalikuta linaongea na msaidizi wake. Lile Jitu lika muuliza binti wewe mtoto unafanya nini hapa? Ondoka. Yule binti akajibu kwa kutaja jina la mama yake na kusema mama anafanyakazi hapa kiwandani kwako naye ni mgonjwa na dakitari anataka dola 50 hivyo nimekuja unipe ili mama yangu apate matibabu. Lile jitu likamwambia yule binti. Hivi wewe mtoto usikii nimesema ondoka upesi kabla sijabadilika. Yule msaidizi wa lile jitu akaanza kuogopa na kutetemeka kwa yatakayoweza kumpata yule mtoto. Yule mtoto akajibu "Hapa sitoki mpaka nimepewa dola 50" Lile jitu likamwambia mtoto nahesabu mpaka tano kama bado upo utanitambua. Mara Jitu likaanza kuhesabu moja, mbili, tatu, nne, tano. Yule mtoto akapaza sauti kwa nguvu sana NATAKA DOLA 50 MAMA YANGU HAWEZI KUFA LAZIMA UNIPE! Lile jitu likasimama na msaidizi wake akawa akitetemeka kwa yatakayompata yule mtoto. Kwa mshangao lile jitu likafungua kabati iliyokuwa pale ofisini akatoa dola 50 akamkabidhi yule binti akamwambia haya chukua nenda kampe mama yako ili akatibiwe umeshinda! Yule binti akawa ameyaponya maisha ya mama yake. Mara nyingi huwa tunashindwa kufikia malengo kwa ajili ya kutovumilia na kutovumilia mara nyingi ni tunda la UOGA au Hofu. Ziko hofu nyingitu, Hofu ya usilolijua, hofu ya kuona watu watasemaje kama nitashindwa na kadhalika. Nakushauri kuanzia leo vumilia na songa mbele kumbuka MVUMILIVU HULA MBIVU Usikate tamaa wewe songa mbele iko siku kila mtu atakuita HERI kila mtu atataka kuwa rafiki yako kwa nini ULIVUMILIA UKAFANIKIWA! ASANTENI. MIKA AYO - MWALIMU

No comments:

Post a Comment