Wednesday, April 20, 2016

JINSI YA KUONGOZA WATU

Habari za leo wasomaji wa makala zangu.
Leo nataka nizungumze kwa kifupi sana jinsi ya kuongoza watu.
Kabla sijaendelea hebu angalia msemo huu wa Kingereza:
A leader's job is not to do the work for others, it's to help others figure out how to do it themselves, to get things done, and to succeed beyond what they thought possible.

― Simon Sinek 

Watu wengi hufikiri kuwa kwa kuwa wamewekwa kuwa viongozi basi wao wanajua kila kitu na wakati mwingine hujikuta wakifanya kila kitu!
 Mwisho wale wanao ongoza hugeuka kuwa watazamaji wa kumwangalia MJUAJI  anaye jua kila kitu akifanya kila kitu hata kama anaharibu wanakaa kimya! Yeye si anajua? Acha afanye mwenyewe.
Nakuomba usiwe hivyo. Kama unataka kufanikiwa katika uongozi waache wengine wafanye wajibu wao halafu unaingia pale watakapoomba msaada ama unapoona kuwa sasa maelekezo mapya yanahitajika.
Usiwe mjuaji, Uwe mtu anayetaka kujifunza na kuwasikiliza wengine ili kuchochea ubunifu na kuwapa unao waongoza mori ya kufanya kazi.
Kwa leo niishie hapa.
Asanteni.
Mika Ayo - Mwalimu 

No comments:

Post a Comment