Friday, April 22, 2016

Leo ni Jumamosi

Wapenzi wasomaji wa makala zangu, Karibuni tena
Leo naomba tujifunze jambo moja kuwa kupumzika haimaanishi kukaa bure bila kufanya kitu.
Nasema hivi kwa sababu watu wengi hutumia siku kama ya leo vibaya kwa jina la KUPUMZIKA! Nataka ujue tu kuwa katika maisha hakuna kupumzika ila tu unabadilisha zoezi moja kwenda jingine. Ukiamua kulala tu mwisho mwili utachoka kulala lazima utaamka tu!
Ukiamua kucheza bao lazima itafika mahali utachoka.
Shida kubwa inakuja pale ambapo tunatumia mapumziko vibaya. Kwa kulewa, kufanya mambo yasiyofaa na kadhalika.
Mimi ningekushauri utumie mapumziko yako kwa kufanya mambo ambayo yataongeza thamani katika maisha yako.
Mfano kwenda kujifunza jambo jipya
Au mtembelee rafiki yako aliyefanikiwa katika jambo fulani ili kubadilishana naye mawazo hata kama kile anachofanya ni tofauti na unachokifanya.
Tumia pesa kwa uangalifu hujui kesho kuna nini Pesa unayoifuja leo kwa mambo yasiyofaa huenda kesho ukaitafuta isiwepo wala asiwepo wa kukupa!
NAWATAKIA WEEK END NJEMA
Mika Ayo - Mwalimu

No comments:

Post a Comment