Friday, April 15, 2016

JINSI YA KUJIONGEZA



Wapenzi  wasomaji wa makala zangu;  habari za leo.
Leo napenda tuzungumze juu ya jinsi ya kujiongeza katika maisha.
Jambo la kwanza kabisa lazima tujue kuwa kila dakika ya maisha yetu inayopita kunamabadiliko yanayotokea kwako, kwa kazi yako au biashara yako. Japo siyo rahisi kuyaona kwa kuwa bado ni mapema kuyaona au kuyatambua, ingawa utakuja kuyaona baadaye! Kuna mwanafalsafa mmoja wa India alisema hivi “unapoanza kuvuka mto kila hatua unayopiga kuvuka mto, ule mto unabadilika na wewe mwenyewe unayevuka unabadilika” .
Alisema kumaanisha kuwa kila sekunde ni sekunde ya mabadiliko. Hivyo tunachotakiwa kukifanya ni kujiongeza ili tuweze kuendana na mabadiliko. Tukichukulia mfano wa mto kubadilika kama ungekaa pale pale ndani yam to kwa muda mrefu kuna siku ungekumbwa na mafuriko. Ndivyo ilivyo katika maisha yetu kama tusipojiongeza tutajikuta tunaathirika na mabadiliko kwa kutojiongeza.
Tunajiongeza kwa kusoma mambo mapya kila siku kuhusu kile tunachokifanya.
Tunajiongeza kwa kuwa wabunifu kuhusu yale tunayoyafanya tujaribu kubuni njia mpya na bora zaidi ya kufanya lile tulifanyalo ili liwe na ufanisi zaidi.
Tunajiongeza kwa kuhakikisha kuwa hatuwanufaishi watu wengine wakati sisi tunazidi kudidimia. Tunawanufaisha waajiri wetu na wanakuwa matajiri wakati sisi tunabaki masikini (simaanishi usitimize wajibu wako kwa mwaajiri na maanisha kuwa hakikisha kuwa na wewe unajinufaisha kwa kuweka mpango wako wa maisha ili usonge mbele).  Tunawanufaisha wauzaji wa bidhaa mbalimbali kwa sisi kuwa wateja na kuridhika na maisha namna hiyo, badala ya sisi nasi kujiongeza na kunufaika kwa kuuza bidhaa zetu ili tubadili maisha yetu.
Kwa mfano wengi wetu tuna simu za mkononi na katika simu hizo tuna watu 250 au zaidi hebu jiulize kati ya hao ni wangapi ni wateja wako? Namaanisha unaofanya nao biashara na kuingiza kipato. Kwa wale ambao angalau watu 10 au zaidi kati ya majina yote yaliyoko kwenye simu yako ni wateja wako nawapa hongera.
Kwa wale ambao bado nawataka mjiongeze, hebu fikiri ni jinsi gani utatumia watu hao kukuingizia kipato badala ya ku- “chat”   tu bila faida yoyote. Fanya kujiongeza kwenye mitandao ya kijamii ambayo wewe unaitumia ili unufaike. Kumbuka hizi zote ni fursa za kupata ushauri juu ya yale tunayoyafanya na pia kupata wateja na kadhalika.
TUJITAHIDI KUJIONGEZA KILA SIKU KWANI KUJIONGEZA KUNAFAIDA KUBWA SANA.
Asanteni.
Mika Ayo – Mwalimu (+255-763506835 au +255-673506836 email mikahezekiel@hotmail.com)

No comments:

Post a Comment